BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MWAMBUNGU MGENI RASMI MASHINDANO YA LIGI DARAJA LA PILI NGAZI YA TAIFA NETBALL.

MKUU wa wilaya ya Morogoro, Saidi Thabiti Mwambungu anatarajia kufungua mashindano ya ligi daraja la pili ngazi ya taifa kwa ajili kutafuta timu nne zitakazopanda na kucheza ligi daraja la kwanza kwa mchezo wa mpira wa pete (Netball) yatayofanyika kufanyika februari 16 katika uwanja wa Jamhuri mjini hapa.

Akizungumza mjini hapa na mwandishi wa habari hizi Kaimu Katibu Mkuu wa chama cha mpira wa pete (Chanemo) Morogoro Rose Joseph alisema kuwa mkuu huyu anatarajia kufungua mashindano ya ligi hiyo ambayo timu 18 zinatarajia kushiriki katika michuano hiyo kwwenye uwanja wa Jamhuri mjini hapa.

Kaimu huyo Rose Joseph alisema maandalizi kwa ajili ufunguzi ya ligi hiyo yamekamilika kwa asilimia 90 na kwamba baadhi ya timu kutoka mikoani zimewasili mkoani hapa ili kuanza kwa kindumbwendumbe kwa kuchuana akinadada hao.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi kutoka chama cha mchezo huo taifa Mary Protasi alithibitisha kwa kuwasili kwa baadhi ya timu saba katika mikoani kuwasili mkoani hapa kwa ajili ya mashindano hayo.

Mwenyekiti huyo alitaja timu zilizowasili kuwa ni JKT Ruvu, Black Sisters kutoka mkoani Pwani, timu ya Hamambe ambayo inamilikiwa na Halmashauri ya jiji la Mbeya, timu ya Rwangwa na Lindi Vijijini kutoka mkoa wa Lindi na timu mwenyeji katika mashindano hayo ambao ni Alance One na Mzinga.

Protasi alitaja baadhi ya timu ambazo zipo njia kuelekea mkoani Morogoro kuwa ni timu ya Tigo Scout za jiji la Dar es Salaam, timu ya Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba na Polisi Pwani.

Timu ya akidada wa jeshi la Polisi Arusha ipo katika hatihati ya kushiriki mashindano hayo kutokana na uongozi kushindwa kutoa uthibisho wa mashindano hayo na kuongeza kuwa mashindano hayo ya mwaka huu yatatarajia kuwa mazuri kutokana na kila timu kupania kuibuka kuwa mabingwa na kuwaomba wakazi wa Manispaa ya Morogoro kujitokeza kwa wingi kwenye uwanja wa Jamhuri kushuhudia mashindano hayo ya pili kwa ukubwa kwa mchezo wa pete hapa nchini.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: