MJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI KLABU YA YANGA SC ANUSURIKA KIFO BAADA YA GARI KUPATA AJALI MOROGORO
Mjumbe wa kamati ya utendaji ndani ya klabu ya Yanga SC, Omary kutoka Zanzibar amenusurika kifo na wenzake wawili baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali eneo la Mwidu barabara kuu ya Dar es Salaam-Morogoro kupinduka.
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa Naipenda YANGA mitandao ya kijamii (facebook) ameleza kuwa gari hilo lilikuwa likiendeshwa na, Sefu Chuma likiwa na mjumbe huyo na abiria mwingine aliyetambuliwa kwa jina la, Bakiri Makere.
Hata hivyo taarifa hiyo imeeleza kuwa watu hao wametoka salama ndani ya gari hilo.
Kupata taarifa hiyo katika ukurasa wa NAIPENDA YANGA bofya maandishi ya chini.
https://www.facebook.com/NinaipendaYANGA/photos/pcb.1323199337722596/1323199191055944/?type=3&theater
0 comments:
Post a Comment