BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

FARASI NDIO MNYAMA HATARI ALIYESABABISHA VIFO VINGI MWAKA 2000 HADI MWAKA 2014


Farasi waliwaua watu wengi zaidi nchini Austrralia miaka ya hivi karibuni kuliko nyoka wote wenye sumu kwa pamoja.

Daktari Ronelle Welton wa Chuo cha Melbourne anasema amechunguza takwimu za watu wanaolazwa hospitalini.

Kuanzia mwaka 2000 hadi 2013 farasi walisabasisha vifo vya watu 74.

Nyuki na wadudu wengine wa kuuma wanakuwa wa pili kama viumbe hatari zaidi, wakisababisha vifo 27 wakifuatiwa na nyoka ambao waliwaua watu 27.

Bui bui hawakusababisha vifo vyovyote wakati wa kipindi hicho.

Utafiti wa daktari Welton unapinga madai kuwa Australia ina wanyama wenye sumu kali.

Lakini kilichotia hofu ni kuwa watu wengi walitafuta matibabu hospitalini baada ya kuumwa na wadudu.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: