BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MASHUA ILIYOBEBA ABIRIA 50 YAZAMA WAKATI IKITOKA TANGA KWENDA PEMBA


Watu kadha wanahofiwa kuaga dunia baada ya mashua iliyokuwa safarini kutoka mji wa bandari wa Tanga ikielekea kisiwa cha Pemba kuzama Jumatatu usiku.

Kamanda polisi eneo la kaskazini mashariki, Benedict Wakulyamba, aliiambia BBC kuwa mashua hiyo ilikuwa imewabeba watu 50.

Mkuu huyo wa Polisi alisema kuwa watu tisa wameokolewa na miili 12 kupatikana.

Kilichosababisha kutokea ajali hiyo hakijathibitishwa lakini kamanda wa polisi anasema upepo mkalia huenda ulisababisha mashua hiyo kupoteza mwelekeo.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: