BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WAFUNGWA WAKATWA VICHWA GEREZANI NA KUPOTEZA MAISHA, POLISI WASHINDWA KUINGIA KUTULIZA VURUGU

Polisi wa kukabiliana na ghasia nchini Brazil wanajaribu kila wawezavyo kuingia ndani ya gereza kuu katika jimbo la Rio Grande do Norte, ambalo limetwaliwa na wafungwa.

Idara ya Polisi inasema kuwa, zaidi ya wafungwa kumi wameuwawa baadhi yao kwa kukatwa katwa katika makabiliano makali kati ya magenge hasimu katika gereza hilo la AlcaƧuz.

Polisi hao wamefika nje ya ukuta wa gereza hilo wakisubiri hadi kutakapopambazuka ndipo waingia ndani.

Mwaka jana pekee zaidi ya wafungwa 100 wamefariki katika makabiliano kama hayo yaliyofanyika awali mwezi huu nchini humo katika magereza yaliyoko katika majimbo ya Amazonas na Roraima.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: