BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

KIKOSI HATARI CHA US NAVY 'SEAL' CHA MAREKANI CHATUA RASMI RASI YA KOREA KUSINI

 

Na Geofrey Chambua 

Yumkini jaribio la mzee wa kiduku limeshtua sana Marekani ambapo sasa ni rasmi Kikosi hatari cha Makomandoo wa Kimarekani ambacho ndicho "The Most Feared Force" katika ulimwengu huu cha US NAVY SEAL inasemekana tayari kiko katika Peninsula ya Korea tangu Jana usiku kikitokea jimbo la Florida nchini Marekani.

Hiki ni kikosi hatari zaidi duniani ambacho kazi yake ni kufanya operations ambazo ni hatari zaidi mno na za mwisho. US Navy Seal ni mjumuisho wa makomandoo hatari zaidi wanaotumia ujuzi wa hali ya juu na wenye mafunzo ya kitaalamu zaidi kuliko makomandoo wengine wa majeshi yote ya kimarekani.

Makomandoo hawa ni wale tu wenye uzoefu wa hali ya juu wa kupambana popote pale iwe angani, ardhini au majini, na katika hali yoyote ile iwe barafu, mvua au jua. Na ndio maana ya neno SEAL ambayo kirefu chake ni Sea, Air and Land.

Ni Mara chache sana kutumika. Hawa ni tofauti na majeshi mengine kama US Army Rangers, US Delta Force na mengine. Katika utawala wa Obama, ametoa ruhusa MARA MOJA tu kwa US Navy Seal kutumika. 


Mara ya mwisho kilitumika usiku wa manane kwa takribani dakika 45 tu kumuangamiza Osama na ni askari mmoja tu alijeruhiwa kwa ajali ya helkopta zisizotoa sauti ambayo ilikosewa ikagonga ukuta wakati makomandoo wakidrop kwenye makazi ya Osama.
Na baada ya Operation Makomandoo hao waliilipua haraka helicopter yao iliyopata hitilafu ili maadui wasigundue teknolojia iliyotumika kutengenezea helicopter hiyo na baada ya kuilipua wakaondoka. Makomandoo wa Navy Seal waliotumika katika Operation hiyo ni 11 tu na Marubani Watatu ambao nao ni kutoka Navy Seal. 


Na ikumbukwe kuwa Operation hii ilikuwa ikitazamwa live (mubashara) kutoka White House ambapo Obama alikuwa akifuatilia (nilirusha tukio hili), kofia za makomandoo hawa zilikuwa na kamera mbele ambazo zilitumika kurekodi kila kitu kinachoonekana mbele na kurusha kwenye satelaiti hadi White House. 
Image may contain: 17 people, people sitting and indoor
Mkakati huu ulisimamiwa na Mwanamke hatari zaidi anayejulikana kama Alfreda Frances Bikosky ambaye ni Afisa mwandamizi wa CIA na jasusi aliyebobea na pia ni komandoo lakini si memba wa Navy Seal. 

Bibi Alfreda anajulikana zaidi katika jeshi la Marekani kama MALKIA WA MATESO. Serikali ya Marekani inajitahidi kudhibiti mitandao ya kijamii na google isisambaze picha za mama huyu hatari.

Kikosi hiki cha US Navy Seal hutumika baada ya makomandoo wengine wa majeshi tofauti ya marekani kusoma Jiografia ya sehem husika, ramani ya ngome za adui na silaha zake then Rais wa Marekani hutoa ruhusa ya NAVY SEAL kutumika kumalizia Operation. 


Baadhi ya majukumu/kazi za Navy Seal ni Direct Operations (kama wanavyotaka kumfanyia North Korea), Strategic Special Missions (kama walivyofanya kwa Osama), Hostage Rescue (kama walivyofanya miaka ya nyuma kuwaokoa Ma-Intelligensia wa Kimarekani waliotekwa Iran) na Foreign Internal Defence.

Mpaka sasa Navy Seal ina jumla ya Makomandoo 8985 ambao ni hatari mno na wenye roho za kinyama. Makomandoo hawa huwa wapo kwenye mazoezi makali ya special operations na trainings ngumu muda wote huko Virginia, Marekani. 

Mara chache sana Navy Seal huwa Recruited kwenda CIA kufanya kazi za Kiintelligensia wanapotakiwa. Makamu wa Rais wa Marekani Bwana Pence yuko Korea Kusini na inasadikika ujio wake umeambatana na NAVY SEAL waliojichimbia katika Nyambizi zisizoonekana katika pwani ya Korea.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: