BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WANASAYANSI WASHINDWA KUWAONA VIUMBE HAI WANAOISHI KATIKA ANGA ZA JUU

Wataalamu wa masuala ya sayansi wanaotafuta maisha katika anga za juu watahitajika kusubiri zaidi.

Mradi huo wa gharama ya dola milioni 100 wa kutafuta dalili za viumbe wa anga za juu bado haujapata chochote mwaka mmoja baada ya kuzinduliwa.

Shughuli hiyo inafanywa kwa kutumia darubini kubwa ambayo inasikiza dalili yoyote ya kuwepo viumbe vya angani.

Wanasayansi walitoa visa 11 ambavyo vilitarajiwa kuonyesha dalili za maisha angani lakini tena wakaamua kuwa vilitoka kwa binadamu. Prof Stephen Hawking anasema kuwa huenda kuna maisha katika anga za juu

Mradi huo ni wa miaka kumi unaoungwa mkono na watu kama Prof Stephen Hawking.

Darubini hizo zina uwezo wa kutafuta dalili za kuwepo teknolojia ambayo iliundwa na viumbe vilivyo nje ya sayari ya dunia. Darubini hii iliyo West Virginia, Marekani ni moja ya darubini zenye nguvu zaidi duniani.

Mwaka uliopita mradi huo ulifuatilia nyota kwa jina Tabby ambayo ilikuwa na tabia iliyosababisha watu wafakiri kuwa ilikuwa na maisha.

Hata hivyo iligunduliwa kwa hali hiyo ilisababishwa na nyota wengine walichangia nyota hiyo kuwa na halili kama hizo. Kiumbe kama huyu anatafutwa
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: