BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

AJALI YAJERUHI 25 WA FAMILIA MOJA MOROGORO


Picha ya maktaba ikionyesha magari yakiwa yamepata ajali ya barabarani.

WATU 25 wa familia moja wamejeruhiwa katika ajali baada ya lori kugongana na basi walilokuwa wakisaifiria.

Ajali hiyo ilitokea jana wilayani Mvomero ambako basi hilo lililogongana na lori namba T 712 CHQ Scania likiwa na tela namba T 591 BYS ambalo lilikuwa likijaribu kuyapita magari mengine.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Urlich Matei, alisema baada ya lori hilo kushindwa kuyapita magari hayo, liligonga basi la Karim Trans namba za usajili T 465 DGQ.

Basi hilo lilikuwa likiendeshwa na dereva Mathew Benedict, likitokea Turiani wilayani Mvomero kwenda mjini Morogoro.

Lilikuwa limekodiwa na familia ya Matesa ambayo ilikuwa ikienda kumaliza msiba wa baba yao.

Kamanda Ulrich alisema majeruhi wengine walitibiwa na kuruhusiwa huku 25 wakilazwa katika Hospitali ya Rufaa Morogoro kwa matibabu zaidi .

“Tumepokea majeruhi wengi lakini wengi wao hawajaumia sana na wametibiwa na kuruhusiwa,” alisema Kamanda Matei

Aliwataja baadhi ya majeruhi walioumia katika ajali hiyo kuwa ni Odilia Ipoliti, Zainabu Mahamba, Shukuru Mrisho, Sauda na Anna ambao wametambulika kwa jina moja.

Kamanda Matei alisema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa lori ambaye alikuwa akijaribu kuyapita magari mengi kwa pamoja na kusababisha ajali hiyo.

“Tunashukuru Mungu hakuna mtu aliyepoteza maisha katika ajali hii.

“Na tunawaomba madereva wote kuwa makini hasa wanapokuwa barabarani wanapoendesha vyombo vya moto,” alisema Kamanda Matei.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: