BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

JE WAJUA SABABU ZA CHUI KULA WINDO LAKE AKIWA JUU YA MTI ?.

Wanyama wengi wakiwemo wanyama wakubwa watano wa Afrika, hurandaranda katika mbuga ya wanyama pori ya Sabi Sand nchini Afrika Kusini.

Wakati mwingine wanyama hawa hupatikana maeneo wasiyotarajiwa, kama twiga mdogo ambaye waelekezi walimpata juu ya mti akiwa amekufa.

Chui mkubwa alimuua twiga huyo kisha akampandisha mita kadha juu ya mti. Alisherehekea chakula hicho kwa siku chache na kuacha tu mifupa, ngozi na nyama nyama zikiwa zimetapakaa.

Twiga huyo alikuwa na uzito wa kila 300 karibu na uzito mara tano zaidi ya Chui. Ikiwa Chui hatompandisha mnyama huyo mtini basi ako kwenye hatari ya kumpoteza kwa fisi na simba.

Ni kitu ambacho kinaeleweka kuwa kisicho cha kawaida kufanyika lakini Chui ana sababu nzuri ya kuweza kufanya hivyo.

Ikiwa Chui hatompandisha mnyama huyo mtini basi ako kwenye hatari ya kumpoteza kwa fisi na simba.

Kumpandisha juu ya mtu humsadia Chui kuzuia chakula chake kuibiwa kwa mujibu wa utafiti uliofanywa mwezi Februari mwaka 2017.

Utafiti uliofanywa na shirika moja lisilokuwa la serikali uligundua kuwa chui katika mbuga ya Sabi Sands huwawinda karibu familia 40 ya wanyama

Chui hupandisha mtini nusu ya wanyama anaowawinda. Pia hupoteza moja ya mawindo yake kati ya matano kwa wanyama wengine kama fisi, simba na hata chui wa kiume.

Ikiwa chui ataamua kupandisha mtini windo lake na kisha kugundua hakuna mshindani karibu anawez kumburura kutafuta mti unaofaa ulio karibu

Mara chuo anapokaribia mti hupanda hadi umbali wa mita10 juu kutafuta eneo lililo salama kuning'inisha windo lake.

Hata hivyo wakati mwingine hali huwa ni ya dharura. Kama fisi yuko karibu Chui mara moja anaweza kupanda mti wowote ulio karibu kuzuia chakula chake kuibwa
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: