BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

KOREA KASKAZINI YAMKAMATA RAIA WA MAREKANI KATIKA CHUO CHA SAYASI NA TEKNOLOJIA CHA PYONGYANG PUST

Kim Hak-song ndiye raia wa nne wa Marekani kukamatwa nchini Korea Kaskazini.

Korea Kaskazini inasema kuwa imemkamata raia wa Marekani kwa kushukiwa kuendesha vitendo viovu dhidi ya taifa hilo.

Kim Hak-song, alikuwa akifanya kazi katika chuo cha sayansi na Teknolojia cha Pyongyang PUST na alikamatwa jana Jumamosi

Raia wengine watatu wa Marekani kwa sasa wanazuiliwa nchini Korea Kaskazini akiwemo Kim Sang-duck, ambaye alikuwa mhadhiri katika chuo cha PUST

Awali Marekani iliilaumu Korea Kaskazini kwa kuwakamata raia wake kuwatumia kwa udhamini.
Kukamatwa mtu huyo kunakuja huku kukishuhudiwa msukosuko kati ya Korea Kaskazini na Marekani.

Korea Kaskazini imetisha kufanya majaribio ya kombora la nuklia huku Marekani nayo ikituma meli ya kivita eneo hilo kuizuia Korea Kaskazini kuunda zana za nuklia.

Kim Hak-song ndiye raia wa nne wa Marekani kukamatwa nchini Korea Kaskazini.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: