BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MVUA ILIVYOLETA MADHARA KWA UPANDE WA MIUNDOMBINU YA BARABARA TANZANIA

Kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha barabara kuu ya Bukoba - Mwanza, Bukoba - Dar es Salaam imekatika katika eneo la Kemondo huku magari yakishindwa kupitia. 

Magari yote ya abiria na mizigo yanayoenda mikoani yanalazimika kuzunguka katika mji wa Kyetema kupitia Katerero na kutokea mbele ya mji huo wa Kemondo na kuendelea na safari. 

Barabara inayotumika kwa sasa imekuwa finyu na magari huku makubwa na mengi yanayopita kuelekea nje ya nchi kupitia mpaka wa Mtukula kwenda Uganda ambapo barabara hiyo sio salama.Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini mkoani Tanga, Steven Ngonyani maarufu kama Prof Maji Marefu akitoa msaada wa kuwaokoa wananchi wa jimbo lake kwenye mafuriko yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mengi ya Tanzania.
Moja ya barabara Visiwani Zanzibar ikiwa imeharibika kwa miundombinu na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: