BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

RAIS JACOB ZUMA ANA SIRI NZITO YA MZEE NELSON MANDELA.


Johannesburg. 
Rais Jacob Zuma anaaminika kuwa na siri nzito ya Rais wa zamani wa nchi hiyo, Nelson Mandela baada ya kufuta safari ya kwenda Maputo, Msumbiji alikokuwa akahudhurie mkutano wa marais wa nchi wanachama wa Ushirikiano wa Maendeleo wa nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).
Zuma alivunja safari hiyo baada ya kumtembelea Mandela hospitalini na kumwona afya yake ikiwa imedhoofika, huku akiendelea kusaidiwa kupum
ua kwa mashine.
Hatua ya Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma kuahirisha safari yake ya Maputo, tayari kumeibua sintofahamu zaidi kuhusu hatima ya afya ya Mandela.
Msemaji wa Rais Zuma, Mac Maharaj alisema kuendelea kuzorota kwa afya ya Mandela ni sababu ya kufutwa kwa safari hiyo.
Hata hivyo, Maharaj akizungumza kwa simu na gazeti hili jana alikataa katakata kuzungumzia undani wa afya ya Mandela, akasema jukumu hilo ni la familia yake na kwamba Ikulu inasaidia tu katika masuala ya jumla yanayohusu afya ya kiongozi huyo.
Familia ya Mandela
Wakati familia ya aliyekuwa mpigania amani na ubaguzi nchini Afrika Kusini, Nelson Mandela wakipeleka mashine ya kuchimbia kaburi katika makaburi ya kifamilia yaliyopo eneo la Qunu, kwa mara ya kwanza, kiongozi huyo amefumbua macho na kurejewa na fahamu.
Taarifa iliyotolewa jana jioni na Ikulu ya Afrika Kusini inasema Rais Zuma alimtembelea Mandela hospitalini mapema jana ambako alipewa taarifa kwamba anaendelea vizuri. “Bado yuko mahututi lakini imara,” ilisema taarifa ya Ikulu na kuongeza:
“Ana nafuu zaidi leo kuliko nilivyomwona jana (juzi) usiku. Timu ya madaktari inaendelea kumtibu.”
Hata hivyo taarifa hiyo ilimnukuu Rais Zuma akilalamikia kile alichosema kuwa ni vyombo vya habari kutoheshimu faragha ya mgonjwa.
Kauli hiyo ya Zuma ilitolewa muda mfupi tangu binti yake Mandela alipovikosoa vyombo vya habari vya nje ya Afrika Kusini, kwamba vinafanya kazi ya kuripoti tukio la ugonjwa wa Mandela katika misingi ya ubaguzi wa rangi.
Akihojiwa na kituo cha televisheni cha SABC jana mchana, Makaziwe alisema kitendo cha vyombo vya Magharibi kuweka kambi nje ya Hospitali ya Medi Clinic alikolazwa baba yake ni kushindwa kuheshimu desturi za Kiafrika.
CHANZO MWANANCHI.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: