MTANGAZAJI wa Kituo cha Televisheni cha ITV Ufoo Saro ambaye Oktoba 13 zilisambaa
taarifa zinazomhusu yeye na familia yake, taarifa hizi zilikuwa za
kupigwa risasi na kujeruhiwa na mzazi mwenzake Anthery Mushi.
Ufoo
saro jana amefanya ibada na kusema ‘Namshukuru Mungu kwa kumponya’ hii
ni mara ya kwanza kwa Saro kuzungumza tukio hilo tangu aliporuhusiwa
kutoka Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu MOI ya Hospitali ya Taifa
Muhimbili alikokuwa amelazwa.
Katika ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheli
Tanzania (KKKT) Usharika wa Kibamba Jimbo la Magharibi Ufoo huku
akitokwa na machozi na wakati mwingine kushindwa kuzungumza alisema ‘Ni
miujiza tu ya Mungu yeye kunifanya mimi kuwa hai leo’.
Mtangazaji huyo ambaye alilazwa kwa zaidi ya wiki mbili hospital
aliwashukuru watu wote waliomtia moyo na kumsaidia kipindi chote
alichokuwa mgonjwa ‘Sina cha kuwalipa,ninawashukuru sana kwa wema wenu
pia kwa kuniombea Mungu ni mkubwa na amenipigania naendelea vizuri kwa
sasa Mungu alinisimamia na nyinyi pia mliniombea hakika sina budi
kushukuru kwa kila jambo,nitasoma zaburi ya 146 katika Biblia Takatifu
ili kumshukuru Mungu kwa kunisaidia’.
Ufoo alisema kuwa ameamua kumshukuru Mungu kwa sababu siyo watu wote wanaopata matatizo kama yake na wakapona.
Mchungaji wa kanisa hilo Joseph Maseghe aliyeongoza misa hiyo
iliyofanyika asubuhi ya leo alisema Mungu hakupanga Ufoo afariki dunia
kwa kupigwa risasi ‘Mungu bado anakuhitaji hakupanga ndiyo maana upo
nasi leo hautakiwi kulia huu ni mwanzo wa maisha yako mengine usilie
unachotakiwa ni kumshukuru Mungu kwa kila jambo’.a;imalizia mchungaji
huyo.
Misa hiyo ilihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwamo wafanyakazi wa ITV
pamoja na Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema) Grace Kihwelu akiwemo na
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) John Heche,baada ya
kukamilika kwa misa hiyo ndugu na marafiki wa karibu wa Ufoo walijumuika
pamoja kwenye hafla fupi ya chakula cha mchana.
0 comments:
Post a Comment