BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MUINGEREZA MWINGINE AKATWA KICHWA NA KUNDI LA WANAMGAMBO WA KIISLAMA LA ISLAMIC STATE SYRIA.


Alan Henning kushoto mda mchache tu kabla ya kukatwa kichwa na mtu aliyesimama kando yake.
Kundi la wanamgambo wa kiislamu la Islamic state limetoa ukanda wa video unaoonyesha mateka Alan Henning raia wa Uingereza akikatwa kichwa.

Henning mwenye umri wa miaka 47 ambaye ni dereva wa texi kutoka kaskazini mwa Uingereza alitekwa nyara mwezi Disemba mwaka uliopita alipokuwa akilifanyia kazi shirika moja la kutoa huduma za misaada kwa wakimbizi nchini Syria.

Kundi la Islamic State ambalo limechukua udhibiti kwenye maeneo ya mpaka kati ya Syria na Iraq tayari lishawaua waandishi wa habari raia wa Marekani James Foley na Steven Sotlof pamoja na mfanyikazi wa kutoa huduma za misaada kutoka Scotland David Haines.

Mapema babake John Cantlie raia wa Uingereza ambaye anashikiliwa mateka na wanamgambo wa Islamic State aliomba kuachiliwa kwa mwanawe.BBC
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: