BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

BURKINA FC YAKUBALI KIPIGO KUTOKA KWA MBEYA CITY LIGI DARAJA LA KWANZA UWANJA WA JAMHURI MOROGORO.

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Mbeya City ya mkoani Mbeya John Kanda kushoto akiwania mpira dhidi ya mlinzi wa Burkina Fc Hamis Omari wakati wa mchezo wao wa ligi daraja la kwanza uliofanyika kwenye uwanja wa Jmahuri mkoa wa Morogoro ambapo katika mchezo huo Mbeya City ilishinda kwa bao 1-0.

 Mlinda Mlango wa Burkina FC ya mkoani Morobgoro Ramadhan Barakati kulia akijiandaa kudaka mpira dhidi ya washambuliaji wa Mbeya City ya jijini Mbeya wakati wa mchezo wao wa ligi daraja la kwanza uliofanyika kwenye uwanja wa Jmahuri mkoa wa Morogoro ambapo katika mchezo huo Mbeya City ilishinda kwa bao 1-0.
TIMU ya ya soka ya Burkina FC imenza vibaya ligi daraja la kwanza baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Mbeya City ya mkoani Mbeya katika mchezo mkali wa ufunguzi wa ligi hiyo uliofanyika kwenye uwanja wa jamhuri na kulala kwa bao 1-0 mkoani Morogoro.
Katika mchezo huo Burkina FC walishindwa kutengeneza mashambulizi ya kutosha kutokana na safu yake ya kiungo kushindwa kutengeneza mipira kwa washambuliaji wao na kuwapa mwanya Mbeya City kutawala eneo hilo.
Mbeya City ndiyo walionekana kutwala mchezo huo kwa vipindi vyote viwili kwa kufanya mashambulizi ya mara kwa mara katika lango la Burkina FC na kuwapa wakati mgumu walinzi na mlinda mlango wa timu hiyo Ramadhan Barakati aliyefanya kazi ya ziada ya kupangua michomo ya washambuliaji wa timu pinzani.
Katika mchezo huo Mbeya City walifanya mashambulizi ya nguvu ya hatari katika lango la Burkina FC katika dakika ya 32, 49 na 50 kwa washambuliaji wake kushindwa kuzifumania nyavu kabla ya kufanya shambulizi lililozaa bao katika dakika ya lililofungwa kiurahisi na nahodha wa Mbeya City Hassan Mwasapili baada ya kuwapiga chenga walinzi na mlinda mlango wa Burkina FC Mohamed Barakati kufuatia pasi ya Hassan Mwasapili.
Burkina FC walifanya shambulizi moja la nguvu ambalo lingezaa kuzaa bao katika dakika ya 21 kwa mpira wa adhabu ndogo nje ya 18 uliopigwa kiufundi na kiungo, Stanley Nyangile na mpira huo kuokolewa na mlinda mlango wa Mbeya City, Aman Simba na kuwa kona ambayo haikujazaa matunda.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: