BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

JESHI LA POLISI YASUSIWA MAITI YA MFUGAJI MOROGORO.

 Baba mzazi wa marehemu, Baya Kidinga (20), Katambi Jidiga kulia akimsikiliza Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile kulia akimweleza jambo juu ya tukio la mauaji ya mtoto wake lililotokea januari 26/ 2013 baada ya kudaiwa askari polisi waliokuwa katika zoezi la udhibiti na ufuatilia kumpiga risasi.
 Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jidai mkoa wa Morogoro Hamis Seleman kulia akimsihi ndugu wa marehemu,Baya Kidinga (20), Madaha Shirinde baada ya kususia maiti mpaka serikali itimize mashrti yaliyowekwa na familia hiyo ndipo wakulibali kuchukua mwili na kuuzika.
 Baba mzazi wa marehemu, Baya Kidinga (20), Katambi Jidiga (katikati) akibembelezwaa na mtoto wake Madaha Shirime kushoto na afisa mtendaji kijiji cha Ipera Asilia, Zikeni Magoha kulia.
 Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Faustine Shilogile kushoto akimsikiliza Manogeleku Kisandu kulia ambaye ni shahidi aliyeshuhudia tukio la kupigwa risasi marehemu Baya Kidinga (20) na askari polisi januari 31/ 2013 katika Kitongoji cha Lugangeni Kijiji cha Ipera Asilia Tarafa ya Mtimbira wilaya ya Ulanga Mkoani hapa.
 Sehemu ya wafugaji wa jamii ya wasukuma wakimsikiliza kamanda wa polisi Morogoro (hayupo pichani) wakati wa tukio hilo.
  Eneo ambalo linadaiwa marehemu Baya Kidinga (20) alipigwa risasi na kufariki dunia baada ya askari polisi kumfyatulia na kupoteza maisha damu ikiwa imetapakaa chini, picha iliyopigwa januari 27/ 2013.
 Marehemu Baya Kidinga (20) enzi za uhai wake.
 Kitambulisho cha marehemu Baya Kidinga (20) cha kuhitimu mafunzo ya Mgambo mkoa wa Morogoro.
 Mmoja wa wafugaji akizungumza jambo mbele ya Kamanda wa polisi hayupo pichani.
 Sehemu kubwa ya wafugaji wilaya ya Ulanga wakimsubiri mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti baada ya familia ya marehemu kukataa kutambua mwili wa marehemu ndugu yao anayedaiwa kupigwa risasi na askari polisi waliokuwa katika zoezi la udhibiti na ufuatilia wa mifugo katika hifadhi ya bonde la mto Kilombero kuupokea na kwenda kuulizika yaliyotolewa na kamanda wa polisi ya mkoa Morogoro huo.
 Mkuu wa wilaya ya Ulanga, Francis Miti kulia akimsikiliza Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Faustine Shilogile kushoto baada ya kamanda huyo kukataliwa na familia ya marehemu Baya Kidinga (20) kutambua mwili wa marehemu kisha kukubali kuupokea na kwenda kuuzika.

 Mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti kushoto akizungumza na wafugaji (hawapo pichani) baada ya wafugaji hao kususia maiti kwa siku mbili wakidai mpaka serikali itimize masharti yaliyowekwa na familia. kushoto ni Kamanda wa polisi Morogoro Shilogile na katikati ni Mwenyekiti wa ccm wilaya ya Ulanga Halidi Nalyoto.

HABARI KAMILI HII HAPA.
JESHI la polisi Wilayani Ulanga Mkoani Morogoro limelazimika kurudisha jumla ya sh 10 milioni zinazodaiwa kuporwa kwa mfugaji wa jamii ya kisukuma baada ya kumuuwa kwa kupigwa risasi mdogoni hatua hiyo ilikuja baada ya kususiwa maiti hiyo kwa siku mbili.

Hatua ya utekelezaji wa urudishaji wa pesa hizo zilizokuwa zikilalamikiwa na ndugu wa mfugaji huyo aliyefahamika kwa jina la Baya Katambi Kidiga ni sehemu ya makubaliano yaliofikiwa mbelee ya Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Francis Mitti na Mkuu wa jeshi la polisi Mkoani hapa Faustine Shilogile, Mkuu wa upelelezi makosa ya jinai mkoani hapa Hamisi Selemani, Mkuu wa polisi Ulanga.

Sakata hilo la mauaji na uporaji linaloendelea kulichafua jeshi la polisi Mkoani Morogoro limetokea tarehe 26, January 2013 katika Kitongoji cha Lugangeni Kijiji cha Ipera Asilia Tarafa ya Mtimbira wilaya ya Ulanga Mkoani hapa.

Awali polisi hao walidaiwa kutekeleza mauaji hayo majira ya saa 4 kwa kumpiga risasi marahemu huyo na kuuchukua mwili wake na kuupeleka kituo cha afya Mtimbira haraka haraka kwa kutumia gari la polisi linalodaiwa likishiriki katika operationi ya kukamata mifugi wilayani humo kutoka kwenye hifadhi ya bonde la mto Kilombero.

Baadhi ya masharti ambayo polisi walitakiwa kutekeleza ni kutoa ripoti ya kina ya uchunguzi wa kifo kutoka kwa daktari ambao utabainisha kuwa marehemu Baya Kidinga (20) amefariki dunia kwa kupigwa kwa risasi.

Hatua ambayo jeshi hilo lilitekeleza kwa kutoa ripoti daktari alitoa riporti ya mauaji hayo yaliodhibitisha bila shaka kuwa ameuwawa kwa kupigwa risasi ambayo ilikubaliwa.

Sharti la pili ambalo polisi walitakiwa kutekeleza ni kujua ni kwanini mwili wa marehemu ulihamishwa toka katika eneo la tukio kwa haraka bila hata kutoa fursa ya ndugu zake kuwepo na baadhi ya ndugu na majirani waliokuwa waliotaka kufuatilia juu ya mkasa huo walizuiwa.

Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alikuwa wa kwanza kuonja makali ya wananchi ambapo aliwasili majira saa saa 5 asubuhi siku ya tukio na jopo la maafisa wa jeshi hili huku idadi ya wafugaji wakiendelea kukusanyika kwa kuulizwa maswali yaliomshinda ikiwemo kutakiwa kueleza kama operationi ya kuwaondoa wafugaji katika hifadhi ya bonde la mto Kilombero ipo au imekwisha na eneo ambalo marehemu ameuwawa ndani ya hifadhi ama laa.

Shilogile akijibu maswali hayo alisema kuwa operationi anachojua yeye ilisitishwa katika wilaya ya Kilombero lakini kwa wilaya ya Ulanga hilo hatakuwa na jibu la swali hilo lakini swahili litajibiwa na mkuu wa wilaya ya Ulanga pindi atapofika.

“Poleni kwa msiba huu mimi nimekuja na timu ya wenzangu akiwemo mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai mkoa wetu lakini natumaini kila kitu kitaenda sawa na kingine mimi nimekuja eneo la tukio kutaka kujua ukweli wa tukio hili ili kubaini ukweli wenyewe ikiwemo nani amefanya kosa na mpaka sasa askari wetu waliohusika katika tukio hilo tayari tunawashikilia kwa ajili ya uchunguzi wa awali na wakibaini sheria itachukua mkondo wake” alisema Shilogile.

Kamanda huyo ambaye alikabiliwa na maswali mengi kutoka kwa wafugaji hao likimwemo la msemaji wa familia hiyo ya marehemu, Baya Kidinga (20), (Madaha Shirinde) aliyeuliza kwa kutaka ufafanuzi wa kina kwa kuuliza swali je askari aliyepata mafunzo anapaswa kufanya nini pindi anapokabiliana na mtu mwenye silaha za asili ikiwemo fimbo ? ama kutuliza ghasia au vurugu anapaswa kutumia bunduki kwa kupiga mwananchi katika eneo gani ?.

Akijibu maswali hayo Kamanda wa polisi Morogoro, Shilogile alijibu kuwa anapaswa kumpiga mtu risasi kwa kutumia bunduki kwenye miguu na kueleza kuwa yeye amefika eneo hilo na timu yake kwa lengo la kujua mazingira ya tukio lililivyofanywa na askari baada ya kufanya uchunguzi na kuwahoji walioshuhudia.

Majibu hayo ya kamanda yalizusha mzogo mkali kutoka kwa wananchi hao na kuzalisha maswali mengine likimo la kuhoji kwanini askari wako ametumia silaha kwa kumpiga marehemu risasi mdogoni kama amepata mafunzo ?.

Kamanda huyo alieleza tena kwa umati wa wafugaji hao kwa kusema kuwa kwa wakati huo atakuwa na jibu la swali hilo na kuongeza hawezi kujua kilichompata askari huyo mpaka ametumia silaha kwa kumpiga risasi marehemu jambo hilo tutalifanyia kazi baada ya kukabilika kwa uchunguzi wao. 

Maswali hayo hayakuweza kuwaridhisha umati wa wananchi na upande wa familia ya marehemu na kumtaka kamanda huyo awasiliane na mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti kwa kuhoji kwa nini wewe Kamanda umetembea umabli mrefu kufika eneo la tukio na mkuu wako wa wilaya ambaye yupo jirani ameshindwa kufika eneo la tukio ?.

Mzozo huo ulidumu kwa muda wa masaa mawili bila kufikia muafaka katika siku ya pili baada ya tukio kutokea ambayo kamanda wa polisi alishindwa kutimiza malengo yake, likiwemo kuwashawishi ndugu wa marehemu wakubali kuutambua mwili wa marehemu, kupokea uchunguzi wa daktari na kuchukua mwili wa marehemu jambo ambalo alilazimika kuwasiliana na mkuu wa wilaya ili kufika eneo la tukio.

DC ULANGA.
Mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti aliwasili katika eneo la tukio la mjira ya saa 10:30 alasiri na kuanza kuwapa pole umati uliokuwa ukimsubiri ili kutatua kero za wananchi hao.

Miti baada ya kutoa pole kwa wafiwa alianza kutoa ufafanuzi juu ya zana iliyojengeka kwa wananchi hao kuwa marehemu amepigwa risasi katika zoezi la operesheni na kuwa askari hao hawakuwa katika operesheni bali walikuwa katika zoezi la udhibiti na ufuatiliaji wa mifugo katika bonde la hifadhi mto wa Kilombero na kuwa wanaobainika hukamatwa na kutozwa faini kisha kuwapa ovyo waliende tena katika bonde la mto Kilombero.

“tukio hili hakuna anayefurahia hata kidogo niwaeleze kuwa operesheni haipo kilichopo sasa ni udhibiti na ufuatiliaji wa mifugo katika bonde la hifadhi mto wa Kilombero na operesheni tayari ilishaisha tangu januari mosi mwaka huu” alisema Miti.

Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya naye alikumbana na maswali juu ya watendaji wake waliokuwa katika operesheni na udhibiti na ufuatiliaji wa mifugo katika bonde la hifadhi mto Kilombero na kuwa daktari wa mifugo wilaya Ulanga, Fredrick Sagamiko amekuwa akidaiwa kukiuka utaratibu wa faini.

Mselengeti Mipawa (41) alimweleza mkuu wa wilaya katika tukio hilo kuwa daktari huyo amekuwa akitoza faini kati ya sh60,000 hadi 100,000 pindi anapokamata mifugo badala ya faini iliyoidhinishwa na serikali ya kiasi cha sh44,000 kwa ng’ombe mmoja jambo ambali wamekuwa wakilipia na kuwarudisha nyumba katika harakati za maendeleo.

Mipawa alimweleza mkuu huyo wa wilaya kuwa daktari huyo wa mifugo wilaya ya Ulanga, licha ya kukiuka utozaji wa faini pia amekuwa akimakata na mifugo ambayo haiku kwenye listi ya ukamataji wa operesheni hiyo wakiwemo kukamata mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na punda na kutozwa faini kubwa kuanzia kiasi cha sh 700,000 na kuendelea kulinagana na uwingi wa mifugo hiyo.

Miti alisema kuwa baada ya kupata tuhuma zinazo mwelekeza daktari wa mifugo wilaya Ulanga, Fredrick Sagamiko yeye atawasilisha tuhuma hizo kwa mwajili wake ambaye ni mkurugezi wa halmashauri ya wilaya ya Ulanga ili uchunguzi ufanyike na kama itabainika sheria itafuata mkondo wake.

Aliwaeleza umati huyo kwa kuwataka wafugaji waache tabia ya kuwashambulia askari na kuwataka askari nayo kutotumia nguvu kubwa wakati wa vurugu pindi inapotokea hiyo itasaidia kuendeleza ushirikiano mzuri baina ya jeshi la polisi na wananchi.

Mkuu huyo alilazimika kuwashawishi ndugu wa marehemu wakubaliane na ombi lao la kutaka wakatambue mwili wa marehemu na kupokea uchunguzi wa daktari kisha kuchukua mwili wa marehemu kwa ajili ya mazishi jambo ambalo lilishindikana kukubali ombi hilo kutokana na kutotimiza madai yao.

Baada ya Kamanda wa polisi na mkuu wa wilaya Ulanga kushindwa kuwashawishi ndugu wa marehemu kuchukua mwili wa ndugu yao msafara wao uliondoka eneo hilo majira ya saa 12:30 jioni na siku ya pili ya januari 28 mwaka huu ikifuatiwa na kutokubaliana hadi gazeti hili liondoka katika eneo la tukio.

Awali Baba wa marehemu Katambi Jidiga alisema kuwa marehemu alitokea mkoani Songea kuuza baadhi ya ng’ombe kwa ajili kulipa madeni ya mifugo iliyokamatwa katika operationi, awali imetajwa mbuzi 100 alilipa lakini saba, ngombe inadaiwa akikuwa akidaiwa 10 milioni na mara ya tatu ngombe wake waliokamatwa na askari hao alikuwa akidaiwa sh milioni 3.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: