BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MKUU WA MKOA APIGWA MAWE KATIKA VURUGU KUBWA CHUO CHA UHASIBU


Mbunge Wa Arusha Mjini Godbless Lema Akiwatuliza Wanafunzi Wa Chuo Hicho
Vurugu  kubwa  zimeibuka  chuo  cha  uhasibu cha Arusha   baada ya mwanachuo kuchomwa kisu na mwanaakijiji na kufariki dunia....

Baada  ya  tukio  hilo, wanafunzi  walitoa  taarifa  kwa  mkuu wa chuo lakini  hakuwapa msaada wowote.
 

Walipokosa  msaada,wanafunzi  hao walianza  kuandamana  na taarifa zikafikishwa kwa mbunge  Godbless  lema .... 


Mbunge  huyo  bila   hiyana akawasili na kufanikiwa kuwatuliza wanachuo hao maana nyumbani kwa Godbless  lema si mbali na chuo hicho ...

Baada  ya  taarifa  kumfikia Mkuu wa mkoa, ilimbidi  aliwasili na kuanza kuzungumza na wanachuo lakini baada ya kugundua uwepo wa Lema alianza kuongea  kwa  lugha  mbovu  na  ndipo wanachuo walipo kasirika na kuanza kumpiga mawe.

Hali  ilipochafuka,FFU  waliingia kazi  ya  kutuliza  ghasia...Hali ni mbaya sana lakini cha kushangaza askari mmoja aliwatonya wanachuo wamfiche Lema

Godbless  Lema  anasakwa mpaka sasana  hajulikani alipo baada ya wanachuo kumficha kusiko julikana.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: