Mama mzazi wa marehemu Albet Mangwea Bi. Denisia Mangwea akisali mbele ya mwili wa mwanae muda mfupi mara baada ya kumalizika kwa zoezi la kuaga kabla ya kuanza msa
fara kuelekea makaburi ya Mtakatifu Monica Kihonda ambapo mazishi yalifanyika mkoani Morogoro jana.
Na Lilian Lucas,Morogoro.
HATIMAYE safari ya mwisho ya
aliyekuwa masanii wa kizazi kipya Albert Magwea maarufu kama Ngwea
imehitimishwa kwa maelfu ya wananchi wa mkoa wa Morogoro, jiji la Dar es salaam
na maeneo mengine ya jirani wamejitokeza kuaga mwili wa msanii huyo baadaye
kushiriki maziko katika makaburi ya kanisa katoliki la mtakatifu Monica
yaliyopo Kihonda mjini Morogoro.
Wananchi hao waliojitokeza kwa wingi
tangu kupokelewa kwa mwili wa msanii huyo siku ya jumatano majira ya saa 11.30
ukianzia maeneo ya Mikese kupitia Msaavu ukitokea Jijini Dar es salaam,
walijitokeza pia katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro ambapo ibada ya
mazishi ilifanyika na baadae watu kuanza kuaga mwili huo.
Hata hivyo mazishi hayo yaliingiliwa na
wasanii wa muziki wa kizazi kipya na wasanii a maigizo ambao walitia dosari,
baada ya baadhi yao kuchelewa kuingia katika uwanja wa Jamhuri, akiwemo
TID, Jini Kabula, Dokii, Juma Nature, na kundi lake na wasanii wengine, kwa
kusababisha kushangiliwa na wananchi waliofika uwanjani hapo.
Aidha magari ya chama chama cha
Mapinduzi nayo yaliingia uwanjani hapo, ingawa hakukuwa na msisimko wa
kushangiliwa kama ilivyojitokeza awali kwa gari lililokuwa na bendera ya chama
cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, hali iliyoonesha wengi waliofka
kuhudhuria msiba huo walikuja kwa nia ya kuwaona wasanii na viongozi wa vyama
vya kisiasa na sio kuomboleza huku na baadhi ya wasaii na vongozi wa kisiasa
wakiingia kwa nia ya kujionesha kwa wananchi.
Hali hiyo ilifanya ibada iliyokuwa
ikiendelea uwanjani hapo ikiendeshwa na Paroko wa kanisa katoliki, Parokia ya
Mt Monica, Octavian Msimbe, kuingiliwa kwa kelele hizo za wananchi mara kwa
mara, ingawa haikusababisha ibada kusimama.
Aidha siku ya kuwasili kwa mwili huo wa
msanii Ngwear kutoka Dar es salam,wananchi pia walisimamisha baadhi ya magari
ya wasanii akiwemo msanii, Dully Sykes, ambaye baada ya kufika eneo la Msamvu
kulikokuwa na mkusanyiko mkubwa wa waananchi, baadhi yao walisimamisha gari
yake na kuzuia isiendelee na safari, huku wakipiga kelele za kuita jina la
Dully na kusukuma gari hiyo kwa mikono.
Akiongea wakati waibada hiyo, Paroko
msaidizi wa Kanisa la St Monica Padre Petter Luanda,aliwataka wananchi
kutohuzunika kwa kupitiliza kuhusiana na kifo cha msanii huyo, kwani wana
nafasi ya kufurahi tena pamoja naye mbinguni, na kwamba kifo hicho ni
kumbukumbu ya kifo cha kila mwanadamu kwa kujiweka tayari kwa vle hawaijui siku
wala saa.
“Hakiwezi kutusubiri tuwe wazee wa
miaka themanini,tunapomsinikiza mwenzetu tujue siku yingine itakuwazamu yetu,
na tujiandae kwa siku hiyo, jiulize kama mimmi ninekufa leo, ningekuaje,
ninngekuwa katika hali ya kukubalika mbinguni au kwenda kwenye adhabu?.
leo ndio
siku ya kufanya uamuzi wa kukiondoa kinachokufanya uende kenye adhabu na
kukufanya kukubalika kwenda mbinguni, tujichunguze sasa uhusiano wetu na Mungu
na kujirekebisha,”Alisema Paroko huyo msaidizi.
Maishi hayo mkoani Morogoro yaliongozwa
na MKuu wa Mkoa Joel Bendera, na waziri Kivuli wa Habari Utaduni na Michezo
kutoka Kambi ya Upinzani Bungeni, Joseph Mbilinyi, Sugu,wawakilishi wa
wizara mbalimbali ikiwemo wizara ya Habari,Utamaduni na michezo, Sugu alisema ifike wakati
Serikali na wadau wegine waangalie maisha ya wasani wakati wa maziko,
yaendane na maisha halisi ya wasanii wakiwa hai.
Mwakilisi wa Mbunge wa Jimbo la Morogoro
Mjini, Mourice Masalla aliwaasa wasanii kutumia msiba huo kuwa na hofu ya Mungu,
huku Msanii Masanja Mkandamizaji alipohojiwa akiwanyumbani kwa marehemu
eneo la Kihonda, akieleza kushangazwa na umati mkubwa ukiojitokeza kumsindikiza
Ngwear na kwamba kama wangekuwa wanajitokeza hivyo wakati wa matamasha na kazi
zao, na kuwaunga mkono, basi huenda umaskini kwa wasanii usingekuwepo.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera,
alieleza Mkoa ulivyopokea kwa msikitiko msiba wa Ngwear akiwa ni kijana mahiri
anayeweza kuigwa na wenzake, na kwamba umati uliojitokeza umeonesha namna
marehemu alivyokuwa karibu na watu, na alivyokuwa karibu na wasanii wenzake na
kuahidi Serikali kuendelea kulinda kazi za wasanii ili waweze kufaidika.
Kwa upande wake katibu mtendaji wa bodi
ya Filamu na mwakilishi wa wizara ya habari,vjana ,utamaduni na michezo Joyce
isso na Kaimu katibu mtendaji wa baraza la sanaa la Taifa BASATA
Godfrey Mngereza walisema serikali inatambua mchango wa Ngwea na kuwaasa
wasanii wanaonuia kuiga mazuri aliyoacha marehemu ikiwa ni pamoja na
kuyaendeleza ili kumuenzi.
Waliwaasa wasanii kuendelea kushirikiana
na serikal katika kuibua,kukuza na kuendeleza vipaji kama cha marehemu angwea
ili muziki na sanaa viendelee mbele,na kuwa njia ya kuwaenzi waasisi wa muziki
na fani nyingine za utamaduni.
Marehemu Albert Keneth Mangwea alizaliwa
mwaka 1982 katika hospitali y Mkoa wa Mbeya, akiwani mtoto wa 10 wa mzee Keneth
Mangwea na mama Denisia mangwea na alipta elimu ya msingi shule ya msingi Bungo
kuazia mwaka 1990, na mwaka 1994 alihamia mkooani Dodoma ambapo alihitimu mwaka
1997 na baadaye alijiunga sekondari ya Mazengo ambapo alihitimu mwaka 2000.
Mwaka 2002 alijiunga na chuo cha sana
Bagamoyo na alikuwa mhamasishaji wa vikundi mbalimbali vya wasanii ikiwemo
kundi la ChembaSquard akiwa kama muasisi wa kundi hilo, na aliasarifi kwenda
nchini Afrika ksini mnamo Machi 26 kwaajili ya shughuli za kimuziki kabla ya
mei 25 alipo0fariki dunia, na kwa mjujibu wa familia ya marehemu, hakuacha mke
wala mtoto.
Mwili wa marehemu Albert Magwear
umezikwa katika makaburi ya kanisa la ST Monica yaliyopo Kihonda katika
Manispaa ya Morogoro.
Hata hivyo taarifa zaidi zilibinisha
Msanii huyo kuwa na mchumba raia wa Canada, ambahye pia alikuwepo katika
mazishi hayo.Bwana ametoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.
Mungu akiweke
roho ya Marehemu Albert mahali pema peponi.

0 comments:
Post a Comment