BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

LIVE MATCH CENTRE: TANZANIA 2-3 VORY COAST MPIRA MAPUMZIKO.


Mpira ni mapumziko. Tanzania 2-3 Ivory Coast 

Zinaongezwa dakika 2 za nyongeza baada ya dk 45 kuisha.

 Yaya Toure anapiga penati Kaseja anapangua lakini mpira unamzidi nguvu na kuzama nyavuni. Tanzania 2-3 Ivory Coast.

Erasto Nyoni anamchezea madhambi Gervinho ndani ya boksi na mwamuzi anaamuru pen
ati.

Mwinyi Kazimoto anapiga shuti kali linalozuiliwa na mkono na beki wa Ivory Coast na inakuwa faulo. Sanata anapiga na inazuiwa na kipa.

Thomas Ulimwengu anaipatia Tanzania goli la kusawazisha akimalizia kazi nzuri ya Shomary Kapombe.

Erasto Nyoni anapiga mpira wa adhabu ambao unadakwa kwa ustadi na kipa wa Ivory Coast.

Thomas Ulimwengu anafanyiwa madhambi na Didier Zakora nje kidogo ya eneo la penati.

Timu zote zinashambuliana kwa kasi ingawa washambuliaji wa Stars wanakosa umakini wakikaribia lango la wapinzani.

Dakika ya 28 - Tanzania 1-2 Ivory Coast

Yaya Toure anapiga faulo nzuri inayotinga wavuni na kuandikia Ivory Coast bao pili.

Kalou anaingia kwenye lango la Stara anachezewa faulo nje kidogo ya eneo la penati.

Dakika ya 21 - Tanzania 1-1 Ivory Coast.

Thomas Ulimwengu na Samatta wanaisumbua ngome ya Ivory Coast.

Taifa Stars wanaonekana kutulia sasa na kupigiana pasi makini katika kutaka kuongeza bao lingine.

Lacina Traore anaisawazishia Ivory Coast
Thomas Ulimwengu anaingia vizuri kwenye lango la Ivory Coast anapiga krosi inayookolewa na Didier Zakora.

Stars wanapata kona ambayo haizai matunda. Dk 5 ya mchezo.

Mpira bado haujatulia timu zote zikipoteza mipira kadhaa ingawa Ivory Coast wanafika zaidi kwenye goli la Stars.

Dakika 3 Ivory Coast wanapata kona ambayo inaokolewa na kuwa mpira wa kurushwa kwenye goli la Stars.

Uwanja wote wa Taifa umefurika mashabiki wakiishangilia kwa nguvu Stars.

Dakika ya 1 kiungo Amri Kiemba anaipatia Tanzania bao la kwanza.

Mpira umeanzaa hapa uwanja wa Taifa

VIKOSI VYA TIMU ZOTE.
Taifa Stars line up: Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Nadir Haroub 'Cannavaro', Kelvin Yondani, Frank Domayo, Mwinyi Kazimoto, Salum Aboubakar 'Sure Boy', Thomas Ulimwengu, Mbwana Samatta na Amri Kiemba

Ivory Coast line up: Barry Boubacar, Boka Arthur, Didier Zokora, Salomon Kalou, Yaw Gervais 'Gervinho', Gosso Gosso Jean Jacques, Aurier Alain, Traore Lacina, Yaya Toure, Serey Geoffroy na Bamba Souleman.
CHANZO  http://www.shaffihdauda.com/
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: