RAIS POUL KAGAME RWANDA KUSHOTO NA RAIS JAKAYA KIKWETE KULIA TANZANIA.MKE WA RAIS WA TANZANIA JAKAYA KIKWETE, MAMA SALMA KIKWETE.
DAR ES SALAAM.
UHUSIANO kati ya Tanzania na Rwanda unazidi kudorora kutokana vyombo vya habari na baadhi ya maofisa wa nchi hiyo kuanza ‘kuichokonoa familia ya Rais Jakaya Kikwete’.
DAR ES SALAAM.
UHUSIANO kati ya Tanzania na Rwanda unazidi kudorora kutokana vyombo vya habari na baadhi ya maofisa wa nchi hiyo kuanza ‘kuichokonoa familia ya Rais Jakaya Kikwete’.
Tovuti ya News of Rwanda, imedai kuwa mke wa Rais,
Salma Kikwete ni ndugu wa kiongozi wa zamani wa taifa hilo, Juvenal
Habyarimana ambaye aliuawa kwen
ye ajali ya ndege wakati akitokea nchini Tanzania mwaka 1993.
ye ajali ya ndege wakati akitokea nchini Tanzania mwaka 1993.
Madai hayo yametokana na mtandao wa Wiki Leaks,
ambao ulinasa mawasiliano kati ya Ubalozi wa Marekani nchini na Serikali
ya nchi hiyo.
Kadhalika taarifa hiyo ya Wiki Leaks imenukuliwa na magazeti mengine ya Rwanda likiwamo gazeti maarufu la New Times.
Kadhalika taarifa hiyo ya Wiki Leaks imenukuliwa na magazeti mengine ya Rwanda likiwamo gazeti maarufu la New Times.
Hata hivyo, Msemaji wa Serikali ambaye ni
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Assah Mwambene amekanusha
taarifa hizo zinazodai kuwa Rais Kikwete ni shemeji yake na Habyarimana.
“Taarifa hizi hazina ukweli wowote na zinalenga kumpaka matope Rais Jakaya Kikwete,” alisema Mwambene.
Mwambene amefafanua kuwa lengo la mitandao ya
kijamii ni kuhabarisha na kuelimisha umma na si kupotosha jamii kwa
kuandika habari zisizo na ukweli wowote.
Kutokana na tovuti hiyo kuchapisha habari hiyo, wasomaji wake walitoa maoni mengi ya kumkashifu Rais Kikwete.
Baadhi yao walikwenda mbali zaidi kwa kuhusisha
habari hiyo na uamuzi wa hivi karibuni wa kuwatimua raia wa Rwanda
wanaoishi bila kibali nchini.
“Kama Mama Salma Kikwete ni binamu wa Habyarimana
basi Rais Kikwete amrudishe nyumbani kwao Rwanda,” aliandika msomaji wa
gazeti hilo, Osma Kanyambo.
Hali hiyo ni mwendelezo wa vita vya maneno kati ya Tanzania na Rwanda, ambavyo vilianza tangu mwezi uliopita.
Chanzo cha hali hiyo ni ushauri uliotolewa na Rais
Kikwete wa kuitaka Rwanda kuzungumza na kundi la waasi la FLDR ambalo
limekuwa likiendesha vita kwa miaka 16 sasa wakiwa mafichoni katika
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Rais Kikwete katika hotuba ya mwisho wa mwezi
uliopita alikiri kudorora kwa uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda na
kwamba nchi hiyo inamshutumu kutokana na ushauri aliowapa. MWANANCHI
0 comments:
Post a Comment