BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HABARI MPYA: YULE MAJERUHI MWANAUME ALIYEPIGWA RISASI NA MFANYABIASHARA, GABRIEL MUNISSI KATIKA KISA CHA MAPENZI AFARIKI DUNIA HOSPITALI YA MUHIMBILI ILALA JIJINI DAR ES SALAAM.


MAJERUHI Francis Shumira aliyejeruhiwa katika tukio la kushambuliwa kwa risasi Ilala Dar es salaam jana amefariki dunia leo asubuhi Hospitali ya Muhimbili alikolazwa MOI kwa matibabu.



Kufariki kwa Francis kunafanya idadi ya watu waliofariki katika tukio hilo hadi hivi sasa huku ikiacha majeruhi wawili mmoja Christina Alfred Newa Mwanafunzi wa masuala ya Mawasiliano visiwa vya Syprus na mama mzazi wa Christina, Hellen Elieza Newa.



Aidha mipango ya mazishi ya mtumishi wa Benki ya Barclays ya jijini Dar es Salaam, Alfa Alfred Newa inafanyika nyumbani kwao Ilala karibu na Kablu ya wazee huku maziko yakisubiri kutengemaa kwa afya ya mama mzazi.
familia imekiri kuwa Christina na Marehemu Munisi walikuwa na mahusiano lakini ni zamani na walitengana kutokana na vurugu alizowahi mfanyia siku za nyuma.

IKUMBUKWE Tukio la shambulizi la risasi lililotokea hii Novemba 19, 2013 asubuhi Ilala Amana jirani na Hoteli ya MM na Klabu maarufu ya wazee limesababisha vifo vya watu wawili na kuacha majeruhi watatu wawili kati yao wakiwa taabani. 



Taarifa za awali za Polisi zinapasha kuwa, Watu walio poteza maisha katika tukio hilo ambalo lilikuwa ni la mtu aliyetambulika kwa jila la Godfrey Munisi kuwapiga risasi wana familia lilisababisha kifo cha Alfa Alfred na liliwajeruhi Francis Khiranga Shumira , Christina Alfred, Hellen Elieza Newa.

Taarifa hizo zinasema kuwa Mfyatua risasi huyo ambaye baade alijiua nayeye, Godfrey Munisi alikuwa na uhusiano wa karibu na Christina Alfred Newa.

Katika tukio hilo, ambalo linaelezwa kuto tofautiana sana na lile la Mwanahabari ufoo Saro lililotokea miezi ya hivi karibuni, muuaji alimjeruhi Nshumila kifuani na mama yake Christina alijeruhiwa maeneo ya begani na hali zao siyo nzuri na wamelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Huku Christina akijeruhiwa mkononi na mguuni ambapo alitibiwa katika Hospitali ya Amana na Kuruhusiwa kurudi nyumbani huku mdogo wa Christina, Alfa Alfred akifariki kabla ya kufikishwa Hospitali.

Marehemu Alfa Alfred Newa pia alikuwa wa benki ya Barclays ya jijini Dar es Salaam. Shumira ni baharia kitaaluma na inaelezwa kuwa ni raia wa Kenya.
CREDIT : MROKIM
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: