BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAUAJI YA KIKONGWE YAIBUA UWANJA WA MPIRA JUU YA KILELE CHA MLIMA MONDO KIJIJI CHA MGATA MOROGORO VIJIJINI.

 
Mchezo wa soka ndiyo mchezo unapendwa zaidi na wapenzi wengi wa michezo mingine duniani na hapa inadhihilisha hilo katika kitongoji cha Gongo kijiji cha Mgata kata ya Bwakilajuu halmashauri ya wilaya ya Morogoro, juu ya kilele cha mlima Mondo unaonekana uwanja wa mchezo wa miguu kwa ajili ya watoto kucheza soka mara baada ya kumaliza shughuli zao hasa zile za masomo ama wikiendi hujazana hapo kusakata kabumbu.


Picha hii ilipigwa Novemba 11 mwaka huu majira ya saa 8 mchana wakati mwandishi wa blog hii akifuatiliwa tukio la mauaji ya kutatanisha ya kikongwe Hellan Petri Mahunzila (75) aliyeuawa kisha mwili wake kutupwa ukiwa umechunwa ngozi kufuatia kutekwa nyakati za usiku oktoba 2/ 2013.

TUKIO hilo la kifo cha kikongwe huyo, Hellan Petri Mahunzila  ambaye alipotea katika mazingira ya kutatanisha kwa siku 12 kisha siku ya 13 mwili wake kuonekana kando ya shamba lake huku maiti yake ikiwa imechunwa ngozi mwili mzima, imezua hofu kubwa na kukubikwa na usiri wa mauaji hayo huku wakazi wa kitongoji cha Gongo kijiji cha Mgata kata ya Bwakilajuu mkoani Morogoro wakiishi kama mnyama digidigi ambaye amekuwa akiwindwa na binadamu kwa ajili ya kitoweo.

MAKALA YA HABARI HIYO INATARAJIWA KUCHAPISHWA KATIKA GAZETI LA MWANANCHI NA MTANDA BLOG HIVI KARIBUNI.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: