BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WATOTO WATATU AMBAO NI WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI WAFA MAJI KATIKA BWAWA LA KUOGELEA JIJINI DAR ES SALAAM.

Daria Mabilo ambaye ni Bibi wa Marehemu, Eva Mwakatobe akifajiwa  na ndugu zake nyumbani kwao Kijitonyama Dar es Salaam jana, Eva ni mmoja wa watoto watatu walifariki Dunia wakati wakisherekea siku ya kuzaliwa rafiki yao iliyofanyika katika Hoteli ya Landmark iliyopo katika ufukwe wa Mbezi. Picha Salim Shao.

Dar es Salaam.
 

Simanzi na vilio jana vilitawala katika Mtaa wa Kijitonyama Mpakani A, baada ya watoto watatu wa familia jirani kufariki dunia baada ya kuzama katika bwawa la kuogelea walipokuwa wakisherehekea siku ya kuzaliwa mtoto mwenzao aliyetimiza mwaka mmoja.
Tukio hilo lilitokea juzi jioni katika Hoteli ya Landmark, Kunduchi Beach Dar es Salaam.


Waliofariki katika ajali hiyo ni Ndimbumi Sisala (9), mwanafunzi wa darasa la nne Shule ya Msingi Kijitonyama, Janeth Kihoko (9) wa darasa la nne Shule ya Msingi Dk Omar Ali Juma na Eva Mwakatobe (11) aliyekuwa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Shekilango.


Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 11:00 jioni.


Tukio lilivyokuwa
Watoto hao walichukuliwa na jirani yao, Anita Mboka kwenda kusherehekea nao siku ya kuzaliwa kwa mtoto wake, Derick Mboka.


Walioshuhudia tukio hilo walisema kuwa baada ya kufika hotelini hapo, watoto walianza kucheza mpira na wengine kuogelea huku mama aliyewapeleka pamoja na wale vijana wakiwa wamekaa wakipata vinywaji.


Kaka wa marehemu Janeth, Goodluck Kihoko (14) alisema yeye na watoto wenzake zaidi ya 20 waliondoka Kijitonyama wakiwa na vijana wanne kwenda kwenye sherehe hiyo.


“Tuliondoka hapa saa kumi na moja jioni, baada ya kufika kule tulianza kuogelea kwenye bwawa, watoto wengine walikuwa wanakwenda kuogelea kwenye maji marefu, walizuiliwa mara tatu, lakini baada ya walinzi kuondoka walirudi na kuzama,” alisema.


Alisema waliona mwili wa Janeth ukielea juu ya maji na kuwaita walinzi ambao waliwapuuza, baada ya muda wakafika na kuona mwili wa pili ukiibuka.


“Tuliwaita walinzi sana, ndipo wakafika na wakati huo mama na wale vijana walikuwa mbali na pale tulipokuwa tukiogelea,” alisema Goodluck.


Mboka hakupatikana baada ya kujifungia nyumbani kwake na majirani walisema ni kutokana na hofu ya msiba huo.MWANANCHI

 
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: