
Pistorius amekana madai ya kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp
Jaji katika kesi ya mauaji ambapo mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius, anashitakiwa kwa kumuua mpenzi wake, ameamuru mwanariadha huyo apelekwe katika kituo cha afya kufanyiwa uchunguzi wa kiakili.
Mnamo Jumatatu, Daktari Bingwa wa akili, aliambia Mahakama kuwa Bwana Pistorius anaugua maradhi yanayaohusiana na kuhangaika.
Jaji alisema kuwa ameridhika kwamba mtaalamu huyo ameshawishi mahakama kuruhusu mshitakiwa kwenda kufanyiwa uchunguzi, ingawa hatua hiyo itachelewesha kuendelea kwa kesi hiyo.
Alisema hatua hiyo hiyo itahakikisha kwamba mshtakiwa anapata haki katika kesi hiyo.
Shahidi mtaalamu - aliyeitwa na upande wa mashitaka - alisema kukatwa miguu yake yote miwili inamweka Pistorius katika hali ambapo akikumbana na tishio atalazimika kujitetea badala ya kutoroka.
Mwanariadha huyo amekiri kumpiga risasi mpenzi wake, Reeva Steenkamp, baada ya kumdhania kuwa jambazi.
Nani aliiba saa za Pistorius?
Saa mbili za kifahari za Oscar Piatorius zilitoweka katika eneo la tukio la mauaji ya mpenzi wake, polisi mstaafu aliifahamisha mahakama inayosikiliza kesi ya mauaji dhidi ya mwanariadha huyo mlemavu.
Polisi huyo kwa jina Schoombie van Rensburg, aliambia mahakama kuwa alikasirishwa sana na kupotea kwa saa hizo na kwamba aliamuru polisi kukaguliwa.
Mahakama pia ilionyeshwa picha ya Pistorius ikiwa amevalia nguo iliyokuwa na damu.
Amekana madai ya kumuua mchumba wake Reeva Steenkamp mwaka jana akisema kuwa alifyatua risasi akidhani jambazi alikuwa amevamia nyumba yake.
Upande wa mashitaka umesema kuwa Pistorius alimuua mchumba wake kwa maksudi baada ya wawili hao kuwa na ugomvi wa kinyumbani mwaka jana.
Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa Jumatatu.
Damu nyumbani kwa Pistorius
Polisi akitoa ushahidi katika kesi inayomkabili Oscar Pistorius.
Kanali Schoombie van Rensburg ameambia mahakama katika kesi inayoendelea dhidi ya Pistorius kuwa alimpata mwanariadha huyo katika hali ya kufadhaika punde baada ya mauaji ya Reeva Steenkamp.
Awali wataalamu wa uchunguzi wa mauaji walitetea polisi kuhusu walivyokusanya ushahidi wao.
Bwana Pistorius amekanusha madai ya kumuua mpenzi wake akisema kuwa alimpiga risasi akidhani alikuwa mwizi ndani ya nyumba yake tarehe 14 mwezi Februari mwaka 2013.
Upande wa mashitaka ulisema kuwa alijaribu kuugonga mlango wa bafu na kisha kufyatua risasi.
Kanali Van Rensburg, aliyekuwa mkuu wa uchunguzi katika tukio la mauaji, alisema kuwa alitoa amri mara moja ya eneo hilo kuzibwa ili uchunguzi uendelee.
Wakili wa upande wa utetezi, Barry Roux amesema kuwa ushahidi kutoka katika eneo la mauaji ulipotea.
Van Rensburg alisema aliona damu kutoka ghorofani ndani ya nyumba ya Oscar pamoja na chembe chembe za damu kwenye viti sebuleni.
Mahakama ilionyeshwa picha za eneo la mauaji ambazo zilionyesha damu kwenye kuta za ghorofa. Kesi hiyo itaendelea hapo kesho Ijumaa.BBC

0 comments:
Post a Comment