BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

YULE MWANAMKE ANAYEHUKUMIWA KUNYONGWA KWA KOSA LA KUOLEWA NA MKRISTO BAADA YA KUACHANA NA UISLAM, SASA AJIFUNGUA MTOTO GEREZANI KULE SUDAN.

sudan 
Yule mwanamke wa Sudan ambaye anasubiri kutumikia adhabu ya kifo baada ya kuisaliti dini yake, amejifungua mtoto akiwa gerezani karibu na mji wa Khartoum kwa mujibu wa mwanasheria wake.

Mwanamke huyo Meriam Yehya Ibrahim Ishag, aliolewa na mwanaume wa kikristu na amehukumiwa kunyongwa mapema mwezi huu baada ya kukataa kuuacha ukristu.

Mwanamke huyo ameruhusiwa kumhudumia mtoto wake huyo wa kike kwa miaka miwili kabla ya kutumikia adhabu hiyo.

Meriam alizaliwa na baba wa kiislamu ambapo ameshtakiwa kwa sheria za kiislamu sharia. Sudan ina idadi kubwa ya watu wa jamii ya kiislamu inayoongozwa na sheria za kiislamu.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: