![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiqpgBvwEgsdFFN28soUmonGmikZk4Q20K0YrTKxET9HCvfFCHNfzEGdcvGwoWHRpCdJqM6hgU05zMKFZwsKeJu_aS07nADMupiD6ehLqWbedskjzXxrs5NNbRCFRAys7e48WpSQBTJwk4/s640/1796530_361143927361551_734923072_n.jpg)
Zikiwa ni takribani wiki tatu tangu tasnia ya muziki wa injili nchini kumpoteza mmoja wa waimbaji wake marehemu mchungaji Debora Saidi, taarifa za kifo cha mwimbaji muziki wa injili Orida Njole zinaeleza kuwa amefariki dunia mchana wa leo katika hospitali ya Temeke jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.
Orida ambaye mpaka umauti unamfika julai 13 mwaka huu ilikuwa bado haijajulikana nini hasa kinamsumbua lakini alikuwa ameishiwa damu sana, mpaka umauti unamkuta alikuwa anatamba na album yake iitwayo 'Duniani tu wapitaji'.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina la Bwana libarikiwe!
0 comments:
Post a Comment