Yanga ilipoteza mchezo wake dhidi ya Mtibwa Sugar uwanja wa Jamhuri kwa kufungwa bao 2-0 huku Ndanda FC ikiisambaratisha Stend United uwanja wake wa nyumbani Shinyanga kwa kuhenyesha kwa kupata ushindi wa bao 4-1 wakati Polisi Moro SC nayo ilikiona cha mtema kuni mbele ya Azam FC kwa bao 3-1 jijini Dar es Salaam.
Mbeya City ilishindwa kuitumia vema uwanja wa Sokoine mbele ya JKT Ruvu kwa kumalizika mchezo kwa sare tasa ya 0-0 wakati Mgambo ilifanikiwa kuifumua Kagera Sugar kwa bao 1-0 mkoani Tanga na Prinson ikaizabua JKT Shooting kwa kuilaza bao 2-1 katika uwanaj wa Mabatini mkoani Pwani.
0 comments:
Post a Comment