BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SAIMON MSUVA AINOGESHA YANGA WAKATI IKIPATA USHINDI KWA JKT MGAMBO 2-0, POLISI MORO SC YAILAZA PRISON, MBEYA CITY HOI SHINYANGA.


Mshambuliaji Saimon Msuva akishangilia moja ya mabao aliyofunga  dhidi ya Mgambo JKT, kushoto ni Ngasa na kulia Dilunga.

Young Africans imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu ya JKT Mgambo ya jijini Tanga katika mchezo uliofanyika jana  Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, huku Saimon Msuva akibuka shujaa kwa kukwamisha wavuni mabao yote mawili.


 

Young Africans iliuanza mchezo kwa kasi kwa lengo la kusaka mabao ya mapema, lakini kutokua makini kwa washambuliaji wake Jaja, Coutinho na Ngasa kulipelekea kukosa mabao ya wazi dakika 45 za kipindi cha kwanza na kufanya timu kwenda mapumziko zikiwa 0-0.

Kipindi cha pili Young African illifanya mabadiliko kwa kuwatoa Haruna Niyonzima na Geilson Santos "Jaja" na nafasi zao kuchukuliwa na Saimon Msuva na Jerson Tegete ambao waliongeza kasi ya mchezo na mashambulizi langoni mwa Mgambo JKT.

Dakika ya 74 ya mchezo, Saimo Msuva aliipatia Young Africans bao la kwanza baada ya kuitendea vyema pasi ndefu ya kiungo Mbuyu Twite aliyompenyezea na kumkuta mfungaji ambaye aliudokoa mpira huo na kujaa wavuni na kumuacha mlinda mlango wa Mgambo JKT Said Lubawa na kujaa wavuni. 


Baada ya bao hilo Mgambo JKT walicharuka na kufanya mashambulizi kadhaa langoni kwa ngome ya Young Africans kwa lengo la kusaka bao la kusawazisha, lakini mashambulizi yao yalikuwa yakiokolewa na walinzi wa Young Africans pamoja na mlianda mlango Deo Munish "Dida".


Huku baadhi ya washabiki wakianza kutoka nje wakijua mchezo umemalizika kwa ushindi wa bao moja, Saimon Msuva tena aliipatia timu yake ya Young Africans bao la pili baada ya pasi aliyotanguliziwa na kiungo Hassan Dilunga kuitumia vyema na kuachikia shuti lililojaa wavuni moja kwa moja. 


Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizka, Young Africans 2 - 0 Mgambo JKT. 



Kwa ushindi wa leo Young Africans inakamata nafasi ya tatu nyuma ya Azam FC iliyoko nafasi ya pili huku wakiwa sawa kwa kwa point na mabao ya kufunga na kufungwa, Mtibwa Sugar wakiendelea kushika nafasi ya kwanza. 



Young Africans: 1. Deo Munish "Dida", 2. Juma Abdul. 3.Oscar Joshua/Hamis Kizza, 4.Rajab Zahir, 5.Kelvin Yondani, 6.Mbuyu Twite, 7.Hassan Dilunga, 8.Haruna Niyonzima/Saimon Msuva, 9.Geilson Santos "Jaja". 10.Mrisho Ngasa, 11.Andrey Coutinho.


Polisi Moro SC kupitia mshambuliaji wao tegemeo Danny Mrwanda aliendeleza kupata ushindi wa pili mfululizo baada ya kuiadhibu Tanzania Prison ya Mbeya kwa bao 1-0 katika mchezo uliofanyika uwanja wa jamhuri Morogoro.

Mrwanda aliipatia timu yake bao pekee katika dakika ya 82 baada ya mlinda mlango wa Tanzania Prison kutema mpira ulioelekezwa langoni kwake na mfungaji kutumia nafasi hiyo kupachika bao.

Stend United nayo ilitumia vyema uwanja wake wa nyumba kwa kuinyuka Mbeya City bao 1-0 mchezo uliofanyika Shinyanga.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: