Msanii wa muziki Rehema Chalamila aka Ray C amefungua mlango kwa mwanaume yoyote anayetaka kumuoa ajitokeze ilimradi awe na vigezo 10 ambavyo ameviainisha. Kupitia ukurasa wake wa instagram Ray C ameandika:
Rehema Chalamila ‘Ray C’
“Habari zenu wapendwa wote dunia nzima! Leo na habari nzuri sana kwenu, Naomba kuwatangazia kuwa natafuta Mchumba wa kuishi nae milele! nataka niwe nae milele na nimzalie watoto wawili wa kike na wakiume!!!!
Ila naomba niwambie kabisa masharti;
1.Awe mpole ili nikikasirika anibembeleze
2.Awe anapenda muvi za kihindi ili nikiwa na stress aniwekee nyimbo za kihindi maana ndio raha ya moyo wangu.
3.Asiwe muongeaji sana sababu huwa sipendi makelele.
4 Anipende na ubonge wangu huu asije akaanza kunambia baby anza mazoezi au dah baby zamani ulikuwa bomba au rudisha kiuno hapo hatutaelewana.
5.Awe ananipikia nikichoka maana navutiwa nikimuona mwanaume anapika.
6.Awe na Mimi muda wote maana na wivu sana ikiwezekana tufanye kazi ofisi moja au awe ofisi ijengwe hapo hapo nyumbani.
7.Awe mvumilivu maana nikiwa na hasira huwa naongea kwa sauti ya juu sana.
8.Asiwe na rafiki wengi na akitaka kuonana nae na mi niwepo maana si mnajua wanaume tena wakikutana huwa wanashaurina mabaya.
9.Awe anajua nyimbo zangu zote ndio ntaamini kweli ananipenda.
10.Sharti la mwisho kabisa ambalo ni muhimu sana kwangu ni hili tuwe tunatumia simu moja na Namba moja, maana kanisani tunafundishwa kuwa ndoa maana yake tumeungana na kuwa kitu kimoja kwahiyo kama mume na mke tunalala pamoja kitanda kimoja na kuishi pamoja kwanini tusitumie simu moja! Sioni tatizo!
Kama una ndugu,jamaa.kaka,rafiki yuko single basi mjulishe tangazo hili huezi jua unaeza ukashangaa nimekuwa shemeji yako au wifi yako”.
HAYA NDIYO MAJIBU ALIYOPATA KATIKA MTANDAO.
-
Sidhani kama mwanamume yoyote atakaye kubali masharti yako, labda wale waliyo zoea kuwekwa na sugar mamy.
Re: Rehema Chalamila Ray C, amefungua mlango kwa Mwanaume yeyote anayetaka kumuoa
Mnavyo mkataa .duh! nahisi anajisikia vibaya sana .khaaa khaaaaa teh teh kwi kwi teh teh
Re: Rehema Chalamila Ray C, amefungua mlango kwa Mwanaume yeyote anayetaka kumuoa
Ruge anamwachia Zamaradi?
Re: Rehema Chalamila Ray C, amefungua mlango kwa Mwanaume yeyote anayetaka kumuoa
Kamnunue supermarket
Re: Rehema Chalamila Ray C, amefungua mlango kwa Mwanaume yeyote anayetaka kumuoa
hahahahahahaaaaaaa aseeeee, ndo wanawake wetu hawa. miaka 15 mpaka ishirini wanaringa mbayaaaaa, 20 mpaka 28 mcharukoooooo hatareeeeeee anajua leo nikiachana na huyu kuna jamaa linatia team sasa hv ye hana shidah.......
30 na kuendelea anaanza kusaka mume ati ...... waru washa lina asali unakuja na mzinga mkavu.... mweeeeeeeh..
Apige moyo konde kuna madingi yanahitaji mke dizain yake.....
cha kumshauri , kwa ndoa za kanisani haipati ng'oooooooo
aslim tu huyu dada waislam wafanye nusra aseeeeeRe: Rehema Chalamila Ray C, amefungua mlango kwa Mwanaume yeyote anayetaka kumuoa
Mh". Wengine mnaponda tu ila moyoni mnalo.
Re: Rehema Chalamila Ray C, amefungua mlango kwa Mwanaume yeyote anayetaka kumuoa
Muda tatizo muda,wanawake hawajui maana ya muda katika maumbile yao.
Re: Rehema Chalamila Ray C, amefungua mlango kwa Mwanaume yeyote anayetaka kumuoa
hata bureeeee simuoiiii...
Re: Rehema Chalamila Ray C, amefungua mlango kwa Mwanaume yeyote anayetaka kumuoa
11. Awe na utaalam wa kung'oa Power Window
-
Re: Rehema Chalamila Ray C, amefungua mlango kwa Mwanaume yeyote anayetaka kumuoa
Teja, wamemaliza kila kitu hadi kule kwenye kampuni la simu, halafu achague mwanaume kwa rundo la masharti ya wakoloni. Yeye, Ray C bwana, mwanaume mtwana! Ama kweli bongo ni sehemu salama ya komedi.
Eti akikasirika abembelezwe! Akiwa na hasira atoe ngurumo ya radi mwanaume unywee! Ukariri na kuimba nyimbo zake mbele yake, asikilize, afurahi mithiri ya malkia! Umpende na huo ubonge wa unga na asifanye mazoezi kwa kuwa uteja ndiyo mpango....! Duh, hakyanani hiyo familia anayoitamani sipati picha.
Kwa hiyo anaoa yeye!!!!!??? -
Re: Rehema Chalamila Ray C, amefungua mlango kwa Mwanaume yeyote anayetaka kumuoa
inamaana anataka kuoa au kuolewa,,,,
1 comments:
Baada ya kuona chapisho kwenye mtandao la Jenna kutoka USA akisema jinsi alivyosaidiwa na Dk. DAWN, niliamua pia kuwasiliana naye kwa msaada kwa sababu sikuwa na chaguo nilichotaka ni kumrudisha mpenzi wangu na furaha. Kwa mshangao mkubwa mpenzi wangu alifika nyumbani akiwa amepiga magoti kwamba nitafute nafasi moyoni mwangu kumsamehe, hakika nilistaajabu na kushtuka mpenzi wangu alipopiga magoti akiomba msamaha na mimi nimkubalie tena. Kweli nimepungukiwa na maneno, na sijui ni kiasi gani cha kukushukuru wewe Dr. DAWN. Wewe ni Mungu aliyetumwa kurejesha uhusiano uliovunjika, Na sasa mimi ni mwanamke mwenye furaha. mawasiliano yake ni Whatsapp +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com
Post a Comment