BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAONI YAANZA KUNG'ATA WAWILI TANZANIA, MAJINA YA JAKAYA KIKWETE FOUNDATION NA TCRA FAUNDATION YAWAPONZA.

 
Wakazi wawili wa jijini Dar es Salam, wamepandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na mashtaka kumi  yakiwamo ya kughushi na kutengeneza tovuti bandia zenye majina ya viongozi mbalimbali akiwemo Rais Jakaya Kikwete.
 
Washtakiwa hao ambao ni Maxmillian Msacky na Patrick Natala wanadaiwa kutengeneza tovuti bandia kwa kudai zinamilikiwa na viongozi Jakaya Kikwete Foundation (Ikulu), Taasisi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA Foundation) na kampuni ya Jamii ya Kuweka na Kukopa ya Akiba (Akiba Saccos Social Company). 
 
Nyingine ni kampuni ya Jamii ya Ridhiwani (Ridhiwani Social Company), Hisa Tanzania, Taasisi ya Zitto Kabwe (Zitto Kabwe Foundation), Vicoba Tanzania na Mfuko wa Wekeza (Wekeza Fund).
 
Mwendesha mashtaka wakili wa serikali mkuu, Theophil Mutakwawa, akisaidiana na Shadrack Kimaro na Jackline Nyatori, walidai katika mahakama hiyo kuwa tarehe tofauti ya mwezi Januari na Aprili, 2014, jijini Dar es Salaam, walitengeneza mfumo wa mtandao uitwao Hisa Tanzania, mahususi kwa ajili ya kulaghai.
 
Katika shtaka la pili washtakiwa wote kwa kutumia miundombinu ya mtandao huo, walitengeneza tovuti ijulikanayo kama Jakaya Foundation, yenye lengo la matumizi ya kulaghai. 
 
Aidha, walitengeneza mfumo wa mtandao uitwao Ridhiwan Social Company,  washtakiwa hao pia walitengeneza mfumo wa mtandao uitwao TCRA Foundation.   
 
Katika shtaka la tano,  tarehe isiyojulikana kati ya mwaka 2001 na 2014 mshtakiwa Msacky akiwa na nia ya kulaghai au kudanyanya, alighushi cheti cha elimu ya Sekondari  namba 0421130 chenye index namba  S02360-0010 akiwa na lengo la kuonyesha cheti hicho kilikuwa halali na kimetolewana Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), huku akijua kuwa si kweli.
 
Ilidaiwa katika shtaka la sita, tarehe isiyojulikana kati ya mwaka 2005 na 2014, mshtakiwa Msacky, alighushi alighushi cheti cha kidato cha sita namba 0217951 chenye index namba S0310-0532, akiwa na lengo la kuonyesha cheti hicho kilikuwa halali na kimetolewa NECTA huku akijua kuwa siyo kweli.
 
Katika shtaka la saba, tarehe isiyojulikana, kati ya mwaka 2006 na 2014, mstakiwa huyo alighushi cheti chenye namba  2004-120202, kwa lengo la kuonyesha cheti hicho kilikuwa halali na kimetolewa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kitengo cha kompyuta.
 
Katika shtaka la nane, tarehe isiyojulikana, kati ya mwaka 2010 na 2014, mshtakiwa huyo akiwa na nia ya kulaghai au kudanganya, alighushi Nakala ya Kitaaluma ikiwa na usajili namba 7703/T.07, kwa lengo la kuonyesha nakala hiyo ilikuwa ni halali na imetolewa na Chuo cha Mzumbe,  huku akijua nim uongo 
 
Mahakama hiyo ilielezwa kuwa, katika shtaka la tisa, tarehe isiyojulikana, kati ya mwaka 2010 na 2014, mshtakiwa huyo, alighushi Cheti cha Chuo chenye namba za usajili 6109 kwa lengo la kuonyesha, cheti hicho ni halali na kilitolewa na chuo cha Mzumbe, wakati akitunukiwa Shahada ya kwanza ya Sayansi katika  Menegimenti ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, huku akijua kuwa si kweli.
 
Katika shtaka la kumi, ilidaiwa kuwa mwezi Julai, 2014 katika ofisi ya SB Enterprises , zilizopo barabara ya Nyerere, jijini Dar es Salaam, mshtakiwa Msacky, kwa nia ya kudanganya, ili kulinda ajira alitoa nyaraka mbali mbali za uongo za vyeti hivyo, kwenye kampuni hiyo, kuonyesha kuwa ni za halali na zimetolewa na mamlaka husika,  huku akijua kuwa taarifa hizo siyo za kweli. 
 
Washtakiwa walikana mashtaka hayo na wamerudishwa rumande hadi Septemba 24, mwaka huu, kesi hiyo itakapotajwa tena.  
SOURCE: NIPASHE
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: