BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HUYU NDIYE SAMAKI ANAYEWEZA KUZALISHA UPYA UTI WA MGONGO WAKE PINDI UNAPOVUNJIKA

Watafiti nchini Marekani wamesema wamebaini aina fulani ya samaki anayeweza kuzalisha upya uti wake wa mgongo unapovunjika wanaweza kusaidia kubuni matibabu yatakayoweza kuwasaidia watu waliopooza kutembea tena.

Wanasayansi wamegundua kuwa samaki huyo ajulikanaye kama Zebra Fish anapovunjika uti wa mgongo, huzalisha sehemu nyingine ya uti wa mgongo na kuunganisha kama daraja sehemu zilizokatika kwa kutumia aina ya protini mwilini mwake.

Wanadamu wanayo aina hiyo ya protini inayoweza kuzalisha mifupa lakini haifanyi kazi sawa na ile ya samaki huyo.

Aina hiyo ya protini kwenye binadamu inafanana kwa asilimia 90 na aina hiyo kwenye samaki hao.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: