BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MFUGAJI APIGWA RISASI KATIKA MAKALIO MKOANI KIGOMA

MFUGAJI na mkazi wa kijiji cha Kagera wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Majibwa Magesa ameuawa baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana wanaotuhumiwa kuwa ni majambazi.

Diwani wa Kata ya Kagera Nkanda, Ezekiel Mshingo amewaambia waandishi wa habari kwamba Magesa aliuawa usiku wa kuamkia jana majira ya saa nane usiku.

Mshingo alisema kuwa Magesa aliuawa baada ya kupigwa risasi katika makalio akiwa katika harakati za kujiokoa.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba watu hao walikuwa wezi.

Kamanda Mtui alisema kuwa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo ingawa wapo watu wanaoshukiwa kuhusika na sasa wamekimbia na polisi inaendelea na upelelezi wa tukio hilo.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: