BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MWANAMKE ALIYE HAI ALALA KWENYE JENEZA ILI KUZOEA MAZINGIRA YA KIFO

Mwanamke aliyekaa siku nzima kwenye Jeneza ili kupata uzoefu wa kifo*

Imetokea *Brazil* na Mwanamke mwenyewe anaitwa *Vera Lucia da Silva* na umri wake ni *miaka 44* ambapo aliamua kukaa kwenye jeneza siku nzima ili apate uzoefu wa mazingira ya kifo ili siku akifa asiwe mgeni na Jeneza.

Vera aliamua kukaa kwenye jeneza huku familia yake ikifanya vitu vinayofanywa kwenye msiba ili aone inakuaje ambapo baada ya kutoka humo alisema ilikua siku nzuri zaidi kwenye maisha yake yote.
*Sherehe hiyo ya kujifunza maisha ya kwenye Jeneza ambayo ilifanyika alhamis  ya November  3 2016 ni sherehe ambayo ilifanyika kwenye eneo la makaburi.*

Ndugu zake walipingana sana na wazo lake lakini baadae waliamua kukubaliana naye na kuvaa nguo nyeusi wakati walipomtembelea na kufanya kama wanatoa heshima za mwisho.

Mmilik wa eneo la kuzikia liitwalo *Eternal Garden Funeral home*, *Paulo Araujo, aliamua kumpa Jeneza Vera bila gharama zozote,* kama mgeni maalumu.*
*Wakati akiwa ndani ya Jeneza mwanamke huyo alikua akifumbua macho na kufumba kama vile mtu aliyekufa na kufufuka.*

*Mwanamke huyo amesema alikuwa na ndoto ya kulala kwenye Jeneza tangu miaka 14 iliyopita na hakuwa akifikiri ingekuja kutokea akaitimiza, kwasasa amefurahi kutimiza alichokitaka kabla hajafa.*

*UKISTAAJABU YA MUSA UTAONA YA FIRAUNI*

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: