BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

NGUO YA NDANI YA MKE WA ADOLF HITLER YAUZWA

Nguo ya ndani ya mke wa Adolf Hitler Eva Braun imeuzwa katika mnada kwa pauni 3000.

Suruali hiyo ikiwa ni miongoni mwa vitu vyengine vya bi. Braun ilipigwa mnada katika jumba la mnada la Phillip Serrell huko Melvern ,ikitarajiwa kuvutia pauni 400 lakini ikauzwa kwa pauni 2,900.

Pete ya dhahabu na kiboksi chenye kioo kilichokuwa na lipstiki nyekundu ya Eva Braun pia kiliuzwa.Vyote hivyo viliuzwa kwa mtu binafsi.


Suruali hiyo ilikuwa na kamba ilikuwa na mapambo ya herufi za Eva Braun.

Pete ya dhahabu iliozungukwa na madini iliuzwa kwa pauni 1,250 huku lipstiki hiyo ya rangi ya fedha ikiuzwa kwa pauni 360.

Wakati huohuo picha za rangi nyeupe na nyeusi za Eva Braun na Adolf Hitler ziliuzwa kwa pauni 100.

Wanaoendesha mnada huo wamethibitisha kuwa ziliuzwa kwa mtu binafsi kutoka Uingereza.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: