BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

PROF MUHONGO AONJA JOTO YA JIWE, NI BAADA YA KUFUKUZWA UWAZIRI NA RAIS MAGUFULI


Rais wa Tanzania John Magufuli amemfuta kazi Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo.

Taarifa kutoka ikulu imesema uamuzi huo wa Rais umeanza kutekelezwa mara moja, na kuwa nafasi hiyo itajazwa baadaye.

Dkt Magufuli amechukua hatua hiyo saa chache baada ya kumshauri Prof Muhongo ajiuzulu.

Rais alitoa wito huo alipokuwa anapokea taarifa ya kamati maalum aliyoiunda kuchunguza mchanga wa madini uliokuwa katika makontena zaidi ya 200 aliyoyazuia yasisafirishwe, kwa ajili ya uchunguzi.

Ripoti iliyowasililishwa katika ikulu ya Tanzania, iliwasilishwa na kamati ya wataalam wa sekta ya madini kubaini aina na kiwango cha madini yaliyo ndani ya mchanga unaosafirishwa kwenda nje.

Katika makontena zaidi ya 200 yaliyokuwa yakichunguzwa, imebainika kuwa yalikuwa na dhahabu yenye thamani ya zaidi ya shilingi Trilioni moja za Tanzania.

Dkt Magufuli alivunja Bodi ya wakala wa ukaguzi wa madini Tanzania TMAA na kumsimamisha kazi Mkurugenzi wake kwa kushindwa kutimiza majukumu yake.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: