BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

FIFA YAIWEKEA NGUVU ZANZIBAR KWA KUIKATAA KAMA MWANACHAMA, YAIPOKONYWA


Zanzibar imepokonywa uanachama wake katika Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) miezi minne baada ya kukubaliwa kuwa mwanachama.

Rais wa Caf Ahmad amesema Zanzibar, ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, haikufaa kukubaliwa kuwa mwanachama wa 55 wa shirikisho hilo mwezi Machi.

"Walipokelewa bila ya kufuatwa kwa sheria za shirikisho ambazo ziko wazi," amesema Ahmad.

"Caf haiwezi kukubalia uanachama wa mashirikisho mawili kutoka kwa taifa moja."

"Ufafanuzi wa maana ya taifa unatoka kwa Muungano wa Afrika (AU) na Umoja wa Mataifa," amesema Ahmad katika mkutano mkuu wa kipekee wa shirikisho hilo nchini Morocco.

Fifa ilikataa kuipokea Zanzibar kama mwanachama hata baada ya hatua ya Caf, iliyoidhinishwa na mtangulizi wa Ahmad, Issa Hayatou.

Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakini imekuwa ikiendesha shughuli zake za soka kivyake na kuwakilishwa katika mashindano ya soka ya kanda.

Zanzibar imepokonywa uanachama wake katika Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) miezi minne baada ya kukubaliwa kuwa mwanachama.

Rais wa Caf Ahmad amesema Zanzibar, ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, haikufaa kukubaliwa kuwa mwanachama wa 55 wa shirikisho hilo mwezi Machi.

"Walipokelewa bila ya kufuatwa kwa sheria za shirikisho ambazo ziko wazi," amesema Ahmad.

"Caf haiwezi kukubalia uanachama wa mashirikisho mawili kutoka kwa taifa moja."

"Ufafanuzi wa maana ya taifa unatoka kwa Muungano wa Afrika (AU) na Umoja wa Mataifa," amesema Ahmad katika mkutano mkuu wa kipekee wa shirikisho hilo nchini Morocco.

Fifa ilikataa kuipokea Zanzibar kama mwanachama hata baada ya hatua ya Caf, iliyoidhinishwa na mtangulizi wa Ahmad, Issa Hayatou.

Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakini imekuwa ikiendesha shughuli zake za soka kivyake na kuwakilishwa katika mashindano ya soka ya kanda.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: