BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

KIONGOZI WA UPINZANI A MGOMBEA URAIS WAKAMATWA NA JESHI LA POLISI

Kabale, Uganda. Mpinzani mkuu wa Uganda na kiongozi wa Forum for Democratic Change (FDC) Dk Kizza Besigye amekamatwa.

Wengine waliokamatwa pamoja na Dk Besigye, ni mgombea urais wa FDC Patrick Amuriat na katibu wa uhamasishaji Ingrid Turinawe. Wote walikamatwa jana jioni walipokuwa katika kijiji cha Burambira, tarafa ya Bubaare, Rubanda walipokuwa njiani wakielekea wilaya ya Kabale wakitokea Rukungiri.

Kamanda wa polisi wa mkoa Denis Namuwoza amesema Besigye anasakwa Rukungiri ambako inadaiwa alitenda makossa kadhaa ya uhalifu Jumatano. “Anatafutwa Rukungiri kwa kutishia kumuua ofisa wa polisi na kuandaa mkutano haramu,” amesema Namuwoza.

Ameongeza kwamba Besigye aliamuru watu kuwarushia mawe maofisa wa polisi ambao walikwenda kutawanya wafuasi wa FDC waliokusanyika kumsikiliza Amuriat aliyekuwemo wilayani kuomba kura.

Walipoondoka kuelekea Kabale saa 11:00 jioni walikutana na kizuizi cha polisi barabarani katika eneo la Burambira, kilomita nne kutoka mjini Kabale. 


Amuriat aliposhuka kwenye gari ili kuzungumza na polisi alikamatwa na kuingizwa kwenye gari la polisi. Kadhalika polisi walizingira gari walilokuwa wakisafiria Besigye na Turinawe.

Wanasiasa hao bado walikuwa wanashikiliwa na polisi hadi saa 1:00 usiku wakati habari hii inaandikwa. “Bado tunamshawishi ashuke kwenye gari ili tumpeleke Rukungiri,” amesema Namuwoza.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: