Dede Ayew ashinda tuzo ya BBC
Dede Andre Ayew 21.
Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Ghana, Black stars na klabu ya nchini Ufaransa,Marseille, Andre 'Dede' Ayew ameshinda shindano la mcheza soka bora wa Afrika mwaka 2011 linaloandaliwa na BBC.
Kijana huyo mwenye umri wa miaka 21 alishinda kwa theluthi ya kura zote zilizopigwa na wasikilizaji na hivyo akifuata nyayo za babake Abedi Pele Ayew aliyeshinda shindano hilo mnamo mwaka 1992.
Ayew alifuatiwa na Yaya Toure wa Ivory Coast na klabu ya Manchester City kwa karibu na pia mchezaji mwingine wa Ivory Coast, Gervinho, Samuel Eto'o wa Cameroon na Seydou Keita kutoka Mali walishindwa.
0 comments:
Post a Comment