Kuku mmoja nchini Marekani ametotoa vitoto vya bata baada ya kutamia mayai ya bata kimakosa.
Kuku huyo aitwaye Hilda, alitamia mayai hayo akidhani ni ya kwake. Gazeti la Daily Mail limesema kuku huyo aliyatamia mayai hayo matano kwa muda wa mwezi mzima, bila kufahamu kama sio ya kuku.
Mmiliki wa kuku huyo, mfugaji Philip Palmer amesema hata kifaranga cha kwanza cha bata kilipotoka, kuku huyohakukata tamaa na aliendelea kutamia na sasa ni kama mama yao.
Mahala pekee kuku huyo anahisi kuna musheli ni wakati vifaranga vya bata vikiingia ndani ya maji na kuku huyo kushinda kuwafuata. Bwana Phillip amesema kuku huyo ameonesha kutojali na vifaranga vya bata hao humfuata kila mahali.
Mfugaji huyo amesema huenda kuku huyo bado hajafahamu kama vifaranga vyake ni bata, na hata vifaranga vyenyewe havijui kama mama yao ni kuku.
0 comments:
Post a Comment