BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

POLISI WADAIWA KUGHUSHI NYARAKA OFISI YA AG

Kwa ufupi
Inadaiwa kuwa nyaraka hizo katika Ofisi ya AG, mkoani Mara, zilighushiwa na askari kanzu mmoja wa Kituo cha Mugumu, ambaye alikuwa akitumiwa na kamanda aliyeondolewa kusaidia mtandao huo, pamoja na mtumishi mmoja wa ofisi hiyo (majina tunayahifadhi kwa sasa). 
GP Said Mwema. 

POLISI wametajwa kuwa miongoni mwa taasisi za dola ambazo zimekuwa zikisaidia kukua kwa vitendo vya ujangili katika hifadhi za taifa, mapori ya akiba na maeneo mengine.

Katika tukio la karibuni, polisi katika Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, wanadaiwa kwamba walighushi nyaraka za Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kuziwasilisha mahakamani kwa lengo la kuwaachia huru watuhumiwa waliokuwa na kesi ya kukutwa na silaha kinyume cha sheria.

Watuhumiwa hao ni wale wanaodaiwa kutumia silaha hizo kwa kufanya uwindaji haramu kwenye mbuga za wanyama kinyume cha sheria, huku mtandao mkubwa walionao katika vyombo vya dola ukichangia vitendo hivyo kuendelea.
Jana gazeti hili lilifichua namna ambavyo baadhi ya mahakimu wamekuwa wakishiriki katika kufanikisha ujangili na biashara ya meno ya tembo na nyara nyingine za Serikali kwa kuwapa watuhumiwa wanaofikishwa mahakanani dhamana na baadaye watuhumiwa hao hutoweka.
Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili ulibaini kuwa baadhi ya watuhumiwa, ambao wamewahi kunaswa na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za ujangili, wametoweka katika njia za kutatanisha na kuacha kesi zikiendelea huku taarifa zikifikishwa mahakamani kwamba watuhumiwa hao wamefariki dunia.
Hata hivyo, mmoja wa watuhumiwa hao Malango Dusara aliyeripotiwa kufariki, anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 3 ya 2010, mkoani Shinyanga kwa kukutwa na risasi 548, amekamatwa tena na sasa yuko mahabusu, baada ya kukutwa akiishi mitaani.
Wakati hayo yakiendelea katika mkondo wa mahakama, baadhi ya polisi wanadaiwa kushiriki uovu huo kwa kuharibu ushahidi wa kesi za watuhumiwa.
Imebainika kwamba, kuharibiwa kwa kesi hizo huanzia kwa polisi, ambao wanaandaa mashtaka na hatimaye mahakamani, ambako inadaiwa watuhumiwa huachiwa na wakati mwingine, hukamatwa tena kwa makosa yaleyale wakiwa nje ya dhamana, lakini bado huachiwa tena.
Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kuwa watuhumiwa wa ujangili akiwamo aliyewahi kutajwa na watuhumiwa wengine kuwa mfadhili wao kutoka Kibondo, mkoani Kigoma, walifutiwa makosa katika mazingira yanayohusishwa na rushwa.
Watuhumiwa hao sita wakazi wa Kigoma, Geita na Tabora ambao walikamatwa katika Kijiji cha Mbirikiri, wilayani Serengeti, mkoani Mara, Mei 12 mwaka huu, wakiwa na  bunduki nne za kivita aina ya SMG  na risasi 436.
Watuhumiwa hao ambao baadaye walifikishwa mahakamani majina tumeyahifadhi, ambapo baada ya kukamatwa walikabidhi silaha ambazo ni SMG mbili walizokuwa wamezificha eneo la Usinge,
Tabora na nyingine mkoani Kigoma na kumtaja mfadhili wao, anayewapa silaha (jina tunalo) ambaye ni mfanyabiashara na mkazi wa Busunzu Kibondo waliyedai anasambaza vijana hifadhi zote za Taifa kwa ajili ya kuua tembo na faru.
Mchakato wa mashtaka
Hata hivyo, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa baada ya kukamatwa mfanyabiashara huyo, kuliibua mvutano baina ya polisi wa mkoani Kigoma na wale wa Mara, ambao walikuwa wakitaka afikishwe Serengeti alikotajwa kwamba anafadhili ujangili, huku wale wa Kigoma wakipinga kwa sababu zisizofahamika.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: