BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

 Wafanyakazi wa mgodi
 Wafanyakazi wa mgodi Afrika Kusini wakigoma.
MR Ian Farmer.

MKURUGENZI mkuu wa kiwanda cha kuchimba madini ya platinum ya Lonmin amejiuzulu, miezi minne baada ya mgomo wa wafanyakazi katika mgodi wake wa Marikani nchini Afrika Kusini, iliyosababisha vifo vya watu 44.

Ian Farmer hajakuwa ofisini tangu mwezi Agosti baada ya kulazwa hospitalini.

Afisa mkuu anayesimamia masuala ya ya fedha Simon Scott, ataendelea kuhudumu kama kaimu afisa mkuu mtendaji wa kampuni hiyo, hadi mridhi wa Bwana Farmers, atakapoteuliwa.

Mgomo wa Marikani uliongeza shinikizo kwa kampuni hiyo ambayo tayari ilikuwa inakabiliwa na kuongezeka ka gharama za utendaji na kushuka kwa bei ya madini ya Platinum.

Kampuni hiyo ambayo imeorodheshwa kwenye masoko ya hisa ya Johannesburg na London, ililazimika kuomba fedha zaidi dola milioni 817 kutoka kwa wenye hisa wake, ili ilishindwe kulipa madeni yake na kukiuka sheria na masharti ya mikopo.

Tarehe kumi na sita mwezi wa nane mwaka huu wafanyakazi 34 wa kampuni hiyo walipigwa risasi na polisi, tukio ambalo lilitajwa kuwa mbaya zaidi tangu kumalizika kwa utawala wa ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini mwaka wa 1994.

Wengine kumi, wakiwemo maaafisa wawili wa polisi waliaga dunia katika maandamano hayo ya wafanyaakazi wa migodi.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: