BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAHAKAMA NCHINI BURUNDI YAMHUKUMU KIFUNGO CHA MIAKA MITATU JELA MWANDISHI WA RFI NA BONESHA FM.



 Mwanahabari wa RFI Kiswahili na Bonesha FM nchini Burundi, Hassan Ruvakuki
Mwanahabari wa RFI Kiswahili na Bonesha FM nchini Burundi, Hassan Ruvakuki.

AFP PHOTO/Esdras Ndikumana.


MAHAKAMA kuu ya Gitega nchini Burundi, leo imetoa  hukumu  ya kifungo cha miaka mitatu  dhidi ya  Mwanahabari wa Radio Bonesha FM na Ripota wa RFIKiswahili Bw Hassan Ruvakuki.

Mawakili wa Ruvakuki wamesema watakata Rufaa, wakionesha kutoridhishwa na humukumu iliyotolewa na Mahakama hiyo.

Chama cha Waandishi wa Habari nchini Burundi UBJ kimelaani vikali hukumu hiyo kikisema kuwa Hassan Ruvakuki hana hatia na hastahili kifungo hicho. 

Wakati Rufaa hiyo inaendelea mwaka jana, Mwendesha mashtaka wa Serikali alisema kuwal, Hassan Ruvakuki alikwenda nchini Tanzania jirani na mpaka wa Burundi ambapo alikutana na Waasi na kufanya Mahojiano nao na kusema kuwa hicho ni kitendo cha uhaini. 

Hassan Ruvakuki na Mawakili wake walibainisha mahakamani kuwa alikwenda kufanya mahojiano na waasi ikiwa ni sehemu ya kazi za kawaida kwa Mwanahabari.

Baadhi ya Raia waliozungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Radio France International wameeleza juu ya matumaini yao kuwa Hassan Ruvakuki ataachwa huru kufuatia mbinyo uliotolewa na Wafadhili wa nje wa Burundi Mwaka jana. 


Hassan Ruvakuki na wenzake walikamatwa na kufungwa mwishoni mwa mwaka 2011, na mara zote mahakamani kumekuwa na mvutano ambapo mwendesha mashtaka wa serikali alishindwa kuthitisha Mashtaka kwa Vielelezo.

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: