Kwa ufupi
“Salamu zangu za Mwaka Mpya kwa Watanzaniaa,
nawaomba wapitishe uamuzi mgumu kwa kila changamoto watakazokabiliana
nazo,” alisema.
LOWASSA.
MAKADA kadhaa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana walikusanyika
jimboni kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kufanya sherehe ya
pamoja ya kuadhimisha Mwaka Mpya.
Habari zilizolifikia gazeti hili zimetaja makada
hao kuwa pamoja na Andrew Change, Beatrice Shelukindo, Peter Serukamba
na Hamis Mngeja ambaye ni Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga.
Akizungumza katika sherehe hizo, Lowassa ambaye ni
Mbunge wa Monduli amewataka Watanzania kutumia Mwaka Mpya kwa kuitisha
uamuzi mgumu.
Akizungumza katika Sherehe za Mwaka Mpya nyumbani
kwake Monduli jana, Lowassa ambaye wafuasi wake wanamwita mzee wa uamuzi
mgumu, alisema kuwa ni muhimu kwa Watanzania kuwa na uamuzi mgumu
katika kila changamoto watakazokabiliana nazo.
“Salamu zangu za Mwaka Mpya kwa Watanzaniaa,
nawaomba wapitishe uamuzi mgumu kwa kila changamoto watakazokabiliana
nazo,” alisema.
Alisema hatua hiyo ni muhimu katika kukabiliana na
umaskini na kuongeza kuwa mtu akiamua inawezekana.
Lowassa katika moja ya mkutano ya Bunge aliitaka Serikali kuwa na tabia ya kupitisha uamuzi mgumu katika kuwaondolea wananchi kero na kumsimamia Rais, alisema bila kuthubutu ni vigumu kukabiliana na changamoto hizo.
Lowassa katika moja ya mkutano ya Bunge aliitaka Serikali kuwa na tabia ya kupitisha uamuzi mgumu katika kuwaondolea wananchi kero na kumsimamia Rais, alisema bila kuthubutu ni vigumu kukabiliana na changamoto hizo.
Lowassa alitumia fursa hiyo kukanusha taarifa zilizozagaa mitandaoni kuwa sherehe yake hiyo ni ya kisiasa akisema:
“Wameandika katika mitandao ya kijamii kuwa kuna
sherehe kubwa ya kisiasa.
Mimi nawaambia waache porojo hizo.
Nimekuwa nikiandaa sherehe hizo tangu mwaka 1995,wao wakitaka waige mfano huu,” alisema Lowassa.
Mimi nawaambia waache porojo hizo.
Nimekuwa nikiandaa sherehe hizo tangu mwaka 1995,wao wakitaka waige mfano huu,” alisema Lowassa.
0 comments:
Post a Comment