BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAMA SALMA KIKWETE APEWA NISHANI YA KAZI ZA WAMA KUTOKA TAASISI YA LONDON UINGEREZA

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania, Mhe. Job Ndugai (kushoto) na Mbunge wa Jimbo la Kilindi (CCM) Beatrice Shelukindo, kwa pamoja wakipokea nishani kwa niaba ya Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, kutoka kwa Dkt. Mohammed Zaharani (katikati yao) kwa wa kwanza (kulia) ni Haruna Mbeyu maarufu kama Meya wa London na anaefuatia ni, Mariam Mungula , Katibu wa Tanzania Women Association (TAWA) UK.

Baadhi ya Akina Mama waKitanzania waliohudhuria hafla hiyo katika picha ya upendeleo na Mhe. Beatrice Shelukindo na Nishati ya Mama Salma .
Akina Mama hao walitamani wote wapande ndege kuelekea jijini Dar Tanzania ili kuikabidhi Nishani hiyo .
****************************
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete, ambaye pia ni Mwanaharakati wa Kijamii kupitia Chama Chake cha Wanawake na Maendeleleo, na Taasisi ya WAMA, wiki iliyopita alizawadiwa Nishani na Chama kinachojishughulisha na kuinua kiwango cha Elimu kwa Nchi za Afrika Mashariki kilichopo jijini London, Uingereza.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo fupi iliyofanyikia katika kumbi za Hoteli ya Park Plaza iliyopo pembeni mwa Westminster Bridge (katikati ya jiji la London) Dkt. Mohammed Zaharan, ambaye ni Katibu wa Chama hicho cha East Africa Education Foundation (EAEF) alisema kuwa Chama Chake kimekuwa kikifuatilia kwa ukaribu shughuli zinazofanywa na Mama Kikwete kupitia Jumuiya ya WAMA ambapo wamefurahishwa na utaratibu wa TAASISI hiyo na kuamua kuitunuku Nishani.

''Tumepata fursa hii ya kumtunukia "Award" kwa kutambua mchango wake mkubwa sana wa kuinua Elimu ya Mtoto, hususan wa kike na vilevile kuwezesha Wanawake ili waweze kujitegemea''. alisema Dkt Zaharani

Aidha Dkt. Zaharani aliongeza kuwa Mama Kikwete ni mfano bora sana wa kuigwa na Wanawake wengine katika jamii ndani na nje ya Tanzania.
Akipokea Nishani hiyo kwa Niaba ya Mama Salma Kikwete, Naibu Spika Mh. Job Ndugai, aliyekuwa Nchini Uingereza kwa Mualiko wa Naibu Spika wa Uingereza na aliyeongozana na Wabunge ambao ni Wajumbe wa Kamati ya Utumishi ya Bunge, alisema kuwa amefurahishwa sana na kitendo hicho cha Mchango wa Mama Salma kuonekana, kwa kuwa kinadhihirisha mchango unaofanywa na Jumuiya zisizo za Kiserikali katika jamii kama WAMA unaonekana mpaka Nje ya Tanzania.
Naye Mhe. Mama Beatrice Shelukindo alifurahi zaidi kwa kitendo tukio hilo na kusema kuwa hili ni jambo kubwa sana na linadhihirisha mchango mkubwa wa Mama Salma katika kumuendeleza Mwanamke wa Kitanzania na inatia moyo kwa Wanawake Wengine.
HONGERA SANA MAMA SALMA NA MWENYEZI MUNGU AZIDI KUKUONGOZA NA KUKUPA AFYA NJEMA ILI UWEZE KUCHANGIA ZAIDI KATIKA MAENDELEO YA MWANAMKE NA MTOTO WA KIKE.
 
CREDITS: SUFIANI MAFOTO
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: