BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MOTO WATEKETEZA BWENI LA WASICHANA SHULE YA SEKONDARI PARAKUYO KILOSA MOROGORO.



Na Juma Mtanda, Morogoro.
MOTO mkubwa umezuka katika bweni la wasichana katika shule ya sekondari ya wafugaji ya Parakuyo na kusabisha hasara baada ya moto huo kuteketeza mali mbalimbali za wanafunzi vikiwemo nguo, madaftari, vitanda na magodoro katika wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini hapa kwa njia ya simu Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kilosa, Ameri Mbaraka alisema kuwa moto huo ulianza majira ya saa 2 usiku wa April 11 mwaka huu na kuteketeza mali za wanafunzi hao ambapo haukuweza kuleta madhala kwa binadamu.

Mbaraka alisema athari kubwa za moto huo ni kutekeza mali zilizokuwemo katika vyumba vya bweni hilo ikiwa ni pamoja na nguo, madaftari, vitanda na magodoro ambapo wanafunzi hao walihamishiwa katika vyumba vya madarasa kwa ajili ya kulala huku juhudi za haraka zikiendelea kufanywa za kuwapatia msaada muhimu.

Msaada ambao unahitajika kwa sasa ni pamoja na magodoro, madaftari, nguo za kushindia na sare, vitanda ambapo moto huo ulizuka wakati wanafunzi wakiwa darasani wakijisome. Alisema Mbaraka.

Mbaraka alisema kuwa juhudi za kuzima moto huo kutoka wa wananchi, walimu na wanafunzi zilishindikana kutokana na kukosa vifaa vya kuzima moto na kushuhudia mali zikiteketea.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa halmashauri hivi sasa inajipanga kuona namna ya kusaidia katika janga hilo na kuweka mikakati ya kuweka vifaa vya kuzima moto katika shule zote za sekondari za wilaya hiyo.

Naye mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo Zuhura Nuiwai alisema kuwa serikali ione namna ya kuwapatia msaada wanafunzi hao kutokana na hasara waliyopata kutokana na moto huo.

Hadi sasa chanzo za moto huo bado hakijajulikana na taarifa zimeelezwa kuwaa wanafunzi watano wamepoteza fahamu kwa mstuko kutokana na tukio hilo na wamelezwa katika hospitali ya Kimamba wilayani humo.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: