Kwa ufupi
“Semdoe alifanya kazi bila kuchoka, alikuwa anafanya
kazi nyingi kwa wakati mmoja, bila manung’uniko, aliweza kufanya habari
lakini wakati huohuo alikuwa akiandika ripoti maalumu,” alisisitiza
Mfalila.
http://www.mwananchi.co.tz
HANDENI:
MWANDISHI wa Habari wa Magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti Wilaya ya Handeni Mkoa wa Tanga, Hussein Semdoe, (37) pamoja na mwenzake wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo, Khamis Bwanga, (53) wamefariki katika ajali ya gari iliyotokea jana katika Kijiji cha Misima, Handeni.
Marehemu Hussein Semdoe akiwa kazini. Picha hii ilipigwa mwishoni mwa wiki Kwamsisi wilayani Handeni mkoani Tanga.
MWANDISHI wa Habari wa Magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti Wilaya ya Handeni Mkoa wa Tanga, Hussein Semdoe, (37) pamoja na mwenzake wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo, Khamis Bwanga, (53) wamefariki katika ajali ya gari iliyotokea jana katika Kijiji cha Misima, Handeni.
Marehemu Hussein Semdoe akiwa kazini. Picha hii ilipigwa mwishoni mwa wiki Kwamsisi wilayani Handeni mkoani Tanga.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo
iliyothibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Costantine Massawe,
mwingine aliyefariki katika ajali hiyo ni Kamishna Mwandamizi wa
Uhamiaji Wilaya ya Handeni, Mariam Hassan.
Kamanda Massawe alisema ajali hiyo ilitokea saa
3:00 asubuhi wakati wakitoka Handeni kwenda Misima kuhudhuria siku ya
upandaji miti.
Katika ajali hiyo, watu watatu walijeruhiwa
akiwemo dereva wa gari hilo, Mtawala Makasi, Sajent Athanas Paul
(Mshauri wa Mgambo Wilaya) na Natolini Mlowe ambaye ni Ofisa Misitu wa
Wilaya ya Handeni. Majeruhi hao wamelazwa katika hospitali ya wilaya
hiyo.
Kamanda Massawe alisema chanzo cha ajali ni
kupasuka kwa tairi la kushoto la gari ambalo liliruka umbali mrefu na
kupindukia porini. Bwanga alirushwa kichakani na kufariki papo hapo
wakati Mariam alifia ndani ya gari. Semdoe alifia Hospitali ya Wilaya
Handeni alikopelekwa kwa matibabu.
Akizungumza jana jioni, Mkuu wa Wilaya ya Handeni,
Muhingo Rweyemamu alisema ofisi yake imepokea kwa masikitiko vifo hivyo
na kuongeza kuwa maziko ya Semdoe ambaye ameacha mjane na watoto wanne,
yatafanyika leo saa nane mchana. Bwanga atapelekwa Muheza.
Kaimu Mhariri Mtendaji Mkuu wa MCL, Bakari Machumu alisema: “Tumesikitishwa sana na kifo cha ghafla cha mwandishi mwenzetu ukizingatia alikuwa katika jitihada za kikazi.”
Kaimu Mhariri Mtendaji Mkuu wa MCL, Bakari Machumu alisema: “Tumesikitishwa sana na kifo cha ghafla cha mwandishi mwenzetu ukizingatia alikuwa katika jitihada za kikazi.”
Machumu alitoa pole kwa familia ya marehemu na
kuiomba iwe na subira hasa katika kipindi hiki kigumu cha majonzi, huku
akiwapa pole waandishi wote wa Mwananchi Mkoa wa Tanga, pamoja na
wafanyakazi wote wa MCL.
Kwa upande wake, Mhariri wa Habari wa Gazeti la
Mwananchi, Samson Mfalila, alisema Semdoe ameacha pengo kubwa katika
chumba cha habari kwani alikuwa mwepesi na mtu aliyejituma katika kazi.
“Semdoe alifanya kazi bila kuchoka, alikuwa
anafanya kazi nyingi kwa wakati mmoja, bila manung’uniko, aliweza
kufanya habari lakini wakati huohuo alikuwa akiandika ripoti maalumu,”
alisisitiza Mfalila.
Mhariri Mtendaji wa Mwananchi Communications Ltd,
Dennis Msacky alisema: “Nimepokea kwa mshituko kifo cha Semdoe kwani
alikuwa kiungo kikuu katika kuhabarisha umma kinachoendelea wilayani
Handeni hasa kwa wananchi wa kawaida.
“Hivi karibuni aliandika ripoti maalumu kuhusu
njaa Handeni na tuliipa nafasi yake,ni pigo kubwa si kwa Mwananchi tu
bali tasnia nzima ya habari.”
Mhariri wa Habari za Mikoani, Tausi Mbowe, alisema Semdoe alikuwa msaada mkubwa katika Mkoa wa Tanga hasa Wilaya ya Handeni.
Mhariri wa Habari za Mikoani, Tausi Mbowe, alisema Semdoe alikuwa msaada mkubwa katika Mkoa wa Tanga hasa Wilaya ya Handeni.
0 comments:
Post a Comment