BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SIMBA YAIBANIA AZAM SC, YATOKA SARE 2-2 LIGI KUU YA VODACOM

Kwa ufupi
Ndoto ya Azam kuisogelea Yanga kileleni imeingia doa jana baada ya kulazimishwa sare 2-2 na Simba iliyoundwa na wachezaji chipukizi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
http://www.mwananchi.co.tz
NDOTO ya Azam kuisogelea Yanga kileleni imeingia doa jana baada ya kulazimishwa sare 2-2 na Simba iliyoundwa na wachezaji chipukizi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mabingwa watetezi Simba walikuwa wa kwanza kupata mabao yao mawili kupitia mshambuliaji wao Ramadhani Singano kabla ya Azam kuamka na kusawazisha mabao kupitia penalti ya Kipre Tchetche na bao lililofungwa na Humpfrey Mieno.
Kwa matokeo hayo Azam imefikisha pointi 47, wakati Yanga wakiwa kileleni na pointi 52, huku Simba wakibaki nafasi ya nne na pointi zao 36 na kupoteza matumaini ya kuiwakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa mwakani.
Katika mechi ya jana, Azam walianza mpira vizuri na kufanikiwa kufika langoni mwa Simba katika dakika ya kwanza baada ya shuti la John Bocco kutoka pembeni kidogo ya goli.
Simba walianza vizuri jibu mapigo baada ya mpira wa kona iliyopigwa na Mrisho Ngassa kutua kichwani mwa Shomari Kapombe, lakini kipa wa Azam, Mwadini Ally alikuwa makini kuokoa hatari hiyo.
Chipukizi Singano aliwainua mashabiki wa Simba kwa kufunga bao la kwanza katika dakika ya 11 akimalizia kazi nzuri ya Ngassa.
Wakati Azam wakiwa hawaamini kinachotokea Singano alifunga bao la pili katika dakika ya 18, baada ya Ngassa kumtoka beki wa Azam, David Mwantika na kupitisha pasi nzuri kwa chipukizi huyo.
Beki wa Azam, Mwantika alionekana mzito na kushindwa kwenda na kasi ya Ngassa na Singano waliomgeuza walivyotaka na kuipa Simba mabao mawili ya haraka.
Baada ya bao hilo kocha wa Azam, Stewart Hall alimtoa Luckson Kakolaki na kumwingiza Hamis Mcha katika dakika ya 20. 

Winga huyo alitumia dakika nane tu kabla ya kuangushwa kwenye eneo la hatari na beki Miraj Mdigo na mwamuzi Oden Mbaga kutoa penalti iliyofungwa na Kipre Tchetche.
Kiungo wa kimataifa wa Kenya, Humpfrey Mieno aliisawazishia Azam bao katika dakika ya 71 akiunganisha vizuri mpira wa adhabu uliopigwa na Mcha baada ya Tchetche kufanyiwa madhambi na Said Nasoro Cholo.
Katika mechi hiyo, mwamuzi Mbaga alimtoa katika benchi, Kocha Hall na kumtaka aende kukaa jukwaani baada ya kumbwatukia akipinga uamuzi wake.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: