Kwa ufupi
Inavyoelekea, Serikali ya Rais Daniel Arap Moi
haikuwa imefurahishwa na jinsi nilivyoripoti mkasa ule. Kumbuka kwamba,
kwa sababu ya hali ya wasiwasi iliyokuwapo nyakati zile, hata magazeti
ya Kenya yenyewe mwanzoni yalikuwa yanapandia kwenye mgongo wa taarifa
zangu nilizokuwa nikizitangaza BBC, Voice of America na Deutche Welle.
http://www.mwananchi.co.tz
Tido Mhando
NI hivi majuzi tu mdau mmoja wa habari, akizungumza
kwenye kikao cha wanahabari alisema: “Mwandishi wa habari ambaye
hajawahi kukabiliwa na kashkashi zozote kwenye kazi yake hiyo, basi ajue
bado hajakomaa.”.
Kauli hiyo ilinikumbusha kasheshe binafsi
iliyonikuta wakati nikiwa bado nchini Kenya, hususan mwaka ule wa 1990
baada ya kuuawa kinyama kwa aliyekuwa waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, Dk
Robert John Ouko.
Kisa ambacho nilikuwa mwandishi wa kwanza wa habari kukitangaza duniani, kama nilivyohadithia kwenye makala zangu tatu zilizopita.
Kisa ambacho nilikuwa mwandishi wa kwanza wa habari kukitangaza duniani, kama nilivyohadithia kwenye makala zangu tatu zilizopita.
Basi kimbelembele changu kile, kidogo kinitokee
puani, kwani wakati nikijibaraguza kwa hili na lile, kumbe wakubwa
walikuwa wananipigia mahesabu ya nguvu.
Inavyoelekea, Serikali ya Rais Daniel Arap Moi
haikuwa imefurahishwa na jinsi nilivyoripoti mkasa ule. Kumbuka kwamba,
kwa sababu ya hali ya wasiwasi iliyokuwapo nyakati zile, hata magazeti
ya Kenya yenyewe mwanzoni yalikuwa yanapandia kwenye mgongo wa taarifa
zangu nilizokuwa nikizitangaza BBC, Voice of America na Deutche Welle.
Kwa kweli hata huko nyuma tayari nilikuwa
nimekwisha tahadharishwa na baadhi ya marafiki zangu (kumbuka nami
nilikuwa nimejijenga vilivyo), kwamba nisipoangalia siku moja nitajikuta
Nyati House, jumba lililopo katikati ya jiji hili na ambalo maafisa wa
usalama walikuwa wanawababazua wapinzani wa serikali, wanaharakati na
hata waandishi wa habari kwa“mateso ya kufa mtu”, ili kujua mambo
wanayoyafanya.
Kwa ujumla, wakati ule wa kilele cha kutaka
mageuzi nchini Kenya, watu wengi nchini humo walikuwa wakiitegemea
zaidi BBC kwa kupata habari za ukweli na uhakika.
Sasa hilo ndilo likawa kosa langu miye niliyekuwa
ripota pekee wa idhaa hiyo nchini Kenya na Afrika Mashariki na Kati kwa
ujumla. Nakumbuka wakati mmoja Rais Moi alipandisha munkari, akawaambia
watu aliokuwa akiwahutubia katika hadhara moja huko Mombasa: “BBC, BBC –
kwani BBC mama yenu ?”.
Sasa mara baada ya kutulia kiasi kwa sekeseke lile
la Dr Ouko, nami nikaanza kupanga ni nini cha kufanya. Kwakweli
nilikuwa nimechoka sana maana kwa kipindi cha zaidi ya miaka mine hivi,
sikuwa nimechukua likizo hata kidogo.
Kama ilivyo kawaida, ukiwa mwandishi wa habari wa
kujitegemea, kula kwako kunatokana na kile unachokikamilisha kila siku,
hivyo muda wa likizo haupo kabisa.
Kwa bahati, Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC ziku
zile, Neville Harms, alikuwa amenialika kwa muda niende London kwa
kipindi cha miezi mitatu ili niweze kuwafahamu vyema wenzangu ninaofanya
nao kazi pamoja na kuyafahamu mazingira yenyewe kwa karibu zaidi.
Akanitumia tiketi, lakini nikawa nimeikalia tu kwani sikuwa na muda huo kwasababu ya kutingwa na kazi nyingi.
Akanitumia tiketi, lakini nikawa nimeikalia tu kwani sikuwa na muda huo kwasababu ya kutingwa na kazi nyingi.
Lakini sasa baada ya kuutua mzigo wa stori ya Dr
Ouko, nikaona heri niitumie ile ofa ya Harms nijiendee London kwa miezi
hiyo mitatu, kiasi iwe kama nimejipumzikia hivi, maana ningekuwa
nafanya kazi ya saa maalum na huku pia nikijipatia muda wa kumpumzika na
kubarizi.
Nikaona huo ni uamuzi wa busara, lakini ilinibidi nijipange na kujitayarisha.
Nikaona huo ni uamuzi wa busara, lakini ilinibidi nijipange na kujitayarisha.
Wakati nikiwa nakamilisha baadhi ya mambo ambayo
niliwajibika kuyawacha vizuri wakati nikiwa sipo kwa muda wote huo wa
miezi mitatu, ikiwa ni pamoja na kurekodi vipindi mbalimbali vya radio
nilivyokuwa nikivitangaza kwa kupitia Sauti ya Kenya (VoK), niliamua
kuchukua siku chache na kwenda Dar es Salaam kuwaaga wazee, maana kama
tujuavyo, unapokwenda dunia ya mbali tena ugenini baraka za wazazi ni
muhimu.
0 comments:
Post a Comment