Kwa ufupi
Vinara hao wa Ligi Kuu, wamewekeza pointi 49 kwenye
msimamo baada ya kushuka dimbani mara 21, ikiiacha Azam FC katika nafasi
ya pili ikiwa na pointi 46.
http://www.mwananchi.co.tz/
http://www.mwananchi.co.tz/
DAR ES SALAAM.
YANGA ina fursa nyingine kulisogelea karibu zaidi taji la ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, lakini hilo likiwezekana tu iwapo wataibuka na ushindi katika pambano lao dhidi ya JKT kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
YANGA ina fursa nyingine kulisogelea karibu zaidi taji la ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, lakini hilo likiwezekana tu iwapo wataibuka na ushindi katika pambano lao dhidi ya JKT kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Vinara hao wa Ligi Kuu, wamewekeza pointi 49
kwenye msimamo baada ya kushuka dimbani mara 21, ikiiacha Azam FC katika
nafasi ya pili ikiwa na pointi 46.
Mahasimu wao na mabingwa watetezi, Simba
wanachechemea kwenye nafasi ya nne wakiwa na pointi 34, ambapo wao
watashuka dimbani kesho kuikabili Azam FC.
Kwa kuzingatia msimamo huo, Yanga ikifanikiwa
kuizamisha Oljoro leo itafikisha pointi 52, ambazo zitaifanya isaliwe na
deni la pointi saba pekee kabla ya kutawazwa mabingwa wapya.
Yanga yenye akiba ya michezo mitano mkononi,
inahitahi ushindi katika mechi zake nne tu mfululizo ikiwamo ya leo
dhidi ya Oljoro ili itwae ubingwa mapema.
Kama dhamira hiyo itafikiwa, basi wafikisha pointi 61 ambazo hazitaweza kufikia na timu nyingine kwenye ligi.
Pamoja yote ,mchezo huo hautakuwa rahisi kwa Yanga
kwa vile Oljoro inayosifika kwa soka la nguvu, itaingia uwanjani kwa
lengo la kulipa kisasi cha kufungwa mchezo wa kwanza.
Katika mchezo wa kwanza mwaka jana kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, Maafande hao walizama kwa bao 1-0.
Oljoro yenye pointi 28 pia inahitaji ushindi utakaoipandisha juu kutoka kwenye nafasi ya nane inayoishikilia kwa sasa.
Kocha wa Yanga, Ernie Brandts amechekelea kurejea
‘vitani’ kwa mshambuliaji wake Jerryson Tegete, ambaye alikuwa nje ya
dimba kwa takriban wiki mbili akiuguza jeraha la goti.
“Tupo tayari kwa mchezo na JKT Oljoro, taarifa
nzuri kwetu ni kurejea kwa Jerryson Tegete aliyeungana nasi asubuhi
kwenye mazoezini ya asubuhi baada ya kupona maumivu ya goti,” alisema
Brandts.
0 comments:
Post a Comment