JANA January 26 kupitia msamalia mwema aliyekua akisafiri toka
Shinyanga kuelekea Morogoro aliwasiliana na millardayo.com na kutoa
taarifa kuhusu kuziba njia kwa madereva wa Malori eneo la Ziba wilaya ya
Nzega Mkoa wa Tabora.
Sababu kubwa za madereva hao wa Malori kufunga barabara ni ile kauli
yao waliyosema kuchoshwa na vitendo vya kutekwa na Majambazi kwenye eneo
hilo,ambapo jana yake January 26 kulitokea kiotendo cha kutekwa kwa
Madereva wa malori huku wakifanyiwa vitendo vya kinyama.
Miongoni mwa vitendo vya kinyama wanavyofanyiwa wanapotekwa ni pamoja
na kupigwa na kuumizwa huku wakihusisha tukio la January 25 ambapo kuna
mtu katobolewa macho,mwingine kakatwa masikio na mwingine kakatwa mguu.
Naomba nikuunganishe na hawa watu watatu walichokisema wa kwanza ni
dereva aliyekuepo eneo hilo wa pili ni Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora
Rpc Peter Charles na Waziri wa Mambo ya Ndani ambaye ameteuliwa hivi
karibuni Mh.Mathias Chikawe.
MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO
Home / Uncategories / BAADA YA KUTEKWA MADEREVA WA MALORI, KAMANDA WA POLISI TABORA NA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI HIKI NDICHO WALICHOSEMA
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment